Jamii FM

Kipindi: NEMC Kanda ya Kusini yaelimisha jamii matumizi mifuko ya plastiki

21 June 2025, 12:01 pm

Maafisa kutoka Baraza la taifa la uhifadhi na usimamizi wa Mazingira NEMC kanda ya kusini wakiwa katika studio za jamii fm Redio zilizopo Naliendele Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Hii ilikuwa sehemu ya kipindi kilichofanyika redioni kuelekea maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani ambapo NEMC iliwasihi wananchi kutumia vifungashio vinavyokubalika kisheria ili kulinda mazingira, huku ikiendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya mifuko ya plastiki na umuhimu wa utunzaji wa mazingira

Na Musa Mtepa

Wananchi wametakiwa kuhakikisha wanatumia vifungashio vinavyostahili kwa ajili ya kulinda na kuhifadhi mazingira, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kitaifa za kupambana na uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na matumizi mabaya ya mifuko ya plastiki.

Hayo yamesemwa na Bi. Nelusigwe Mwanjabeki, Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kanda ya kusini, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na 90. Jamii FM Redio.

Amesema NEMC inaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi sahihi ya vifungashio kupitia kampeni mbalimbali katika masoko na vyombo vya habari, ili kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na uelewa sahihi kuhusu utunzaji wa mazingira.

Sauti ya 1 Nelusigwe Mwanjabeki afisa ustawi wa jamii mwandamizi NEMC

Bi. Nelusigwe ameongeza kuwa vifungashio vinavyofaa ni vile vilivyo na alama za ubora na maelezo ya bidhaa kama vile sukari, chumvi na vinginevyo vinavyoonyesha mzigo halisi unaobebwa pamoja na nembo ya utengenezaji.

Sauti ya 2 Nelusigwe Mwanjabeki afisa ustawi wa jamii mwandamizi NEMC

Akijibu swali kutoka kwa msikilizaji aliyependa kufahamu mikakati ya kufikisha elimu ya mazingira hadi vijijini, Bi. Nelusigwe amesema  kumekuwa na vitu mbalimbali vinavyofanywa ili kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa juu ya matumzi ya mifuko ya plastiki na athari zake.

Sauti ya 3 Nelusigwe Mwanjabeki afisa ustawi wa jamii mwandamizi NEMC

Kwa upande wake, Bw. Muungano Senyagwa, Afisa Mazingira kutoka ofisi ya NEMC kanda ya kusini, amesisitiza kuwa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki lipo kwa mujibu wa sheria, kama ilivyoelezwa katika tangazo la serikali lililotolewa tarehe 1 Juni, 2019 kupitia Gazeti la Serikali.

Sauti ya Muungano Senyagwa afisa mazingira NEMC kanda ya kusini.