Jamii FM

Jamii yatakiwa kuelewa umuhimu wa malezi ya watoto

20 June 2024, 18:56 pm

Baadhi ya waandishi wa habari mkoani Mtwara wakiwa katika mafunzo  ya siku moja juu ya masuala ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) yaliyofanyika   19.6.2024 katika ukumbi wa TCCIA mkoani hapa(Picha na Mwanahamisi Chikambu)

Uelewa wa jamii juu ya masuala ya malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kwa wenye umri wa miaka 0-8 ni jambo muhimu katika kuirejesha jamii katika mstari wa malezi sahihi ya watoto.

Na Mwanahamisi Chikambu

Uelewa juu ya masuala ya malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto wenye umri wa miaka 0-8 ni jambo muhimu katika kuirejesha jamii katika mstari wa malezi sahihi ya watoto nchini.

Hayo yameelezwa na Edwad Biashara ambaye ni mkufunzi wa program ya malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto katika mafunzo  ya siku moja kwa waandishi wa habari katika masuala ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) mkoani Mtwara yaliyofanyika jana  19.6.2024 katika ukumbi wa TCCIA mkoani hapa.

Sauti ya Edward Biashara mkufunzi wa mafunzo kwa Waandishi wa habari

Kwa upande wake afisa ustawi wa jamii kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara ambae pia ni mratibu wa program ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Teresia Ngonyani  ameiomba jamii kuwekeza kwa watoto kuanzia umri wa miaka 0-8 ili kuhakikisha watoto hao wanakuwa katika ukuaji timilifu  na kuwapa matunzo na malezi bora.

Sauti ya Teresia Ngonyani afisa wa ustawi wa jamii kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa

Wakizungumza mara baada ya mafunzo hayo baadhi ya waandishi  wa habari kutoka mkoani mtwara waliohudhuria katika mafunzo hayo wamesema kwamba kutokana na elimu waliyoipata watakwenda kuelimisha jamii juu malezi makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto.

Sauti ya Zam zam Jambia na Omari Mikoma waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo hayo kutoka mkoa wa Mtwara

Programu Jumuishi ya Kitaifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ilizinduliwa Dodoma na aliyekuwa waziri wa Afya kipindi kile Dk Dorothy Gwajima kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hasaan mwaka 2021.