Jamii FM

Makala – Elimu ya Usalama Barabarani kwa Watu Wenye Ulemavu

20 June 2024, 16:00 pm

Moja ya alama za barabarani zilizopo katika barabara kuu ya kutoka mkoa wa mtwara kuelekea mikoa mingine , alama zipo eneo la Pacha ya Mbae. Picha na Msafiri Kipila

Watu wenye ulemavu wanasisitiza umuhimu kwa watumiaji wa barabara kuwapa kipaumbele kutokana na changamoto wanazokutana nazo wanapotumia barabara. Kila mmoja wetu ana jukumu la kuhakikisha usalama barabarani, si jukumu la serikali pekee.

Abeid Yusufu Lukanga, ambaye ni mlemavu anayetumia baiskeli, ameeleza kuwa alama zinazowatambulisha watu wenye ulemavu zipo lakini baadhi ya madereva wanashindwa kuzitambua. Hii ni hatari kwa usalama wao wanapokuwa barabarani.

Mkaguzi msaidizi wa jeshi la Polisi Rebeca Milele akimuelezea Muandaaji wa makala hii Msafiri Kipila alama mojawapo ya watu wenye ulemavu. picha na Musa Mtepa

Mkaguzi msaidizi wa jeshi la Polisi Rebeca Milele kutoka ofisi ya usalama barabarani mkoa wa Mtwara amethibitisha kwamba wanatoa elimu ya usalama barabarani kupitia shule na vyombo vya habari ili kuhakikisha kuwa kila mtu, ikiwemo watu wenye ulemavu, wanafikiwa na elimu hiyo.

Tushirikiane kupunguza ajali za barabarani na kuokoa maisha ya watu wenye ulemavu. Kusikiliza makala hii kutakusaidia kuelewa zaidi.

Bonyeza hapa