Jamii FM

Jamii Africa yawajengea uwezo Waandishi wa habari Mtwara

18/03/2026, 08:49

Waandishi wa habari wakiwa katika mafunzo ya utambuzi na uthibitishaji wa taarifa yaliyotolewa na Jamii Africa yaliyofanyika March 17,2026 mjini Mtwara(Picha na Hery Abdala)

Waandishi wa habari 25 mkoani Mtwara wamepata mafunzo ya uhakiki wa taarifa kutoka Jamii Africa, yakilenga kuwasaidia kutambua taarifa sahihi na potofu ili kuboresha utoaji wa habari kwa wananchi

Na Musa Mtepa

Jumla ya waandishi wa habari 25 kutoka vyombo mbalimbali mkoani Mtwara wamepatiwa mafunzo ya uhakiki na uthibitishaji wa taarifa, yaliyotolewa na Jamii Africa chini ya taasisi mama ya Jamii Forums, kwa lengo la kuwawezesha kutambua taarifa potofu na zisizo sahihi katika jamii.

Wakizungumza baada ya mafunzo hayo yaliyofanyika Machi 17, 2026 mjini Mtwara, waandishi hao wameishukuru Jamii Africa kwa kuwapatia mafunzo hayo, wakisema yatawasaidia katika kazi zao za kila siku za kuhabarisha wananchi.

Aidha, waandishi hao wamesema kutokana na kukua kwa teknolojia, kumekuwa na changamoto ya watu kuzalisha maudhui ambayo kwa namna moja au nyingine husababisha mkanganyiko wa kutambua taarifa sahihi na zisizo sahihi hivyo, kupitia mafunzo hayo, wataweza kubaini ipi ni taarifa sahihi na ipi si sahihi.

Sauti ya Waandishi wa habari Mtwara

Naye Afisa Programu kutoka Jamii Africa, Edward Chaina, amesema mafunzo ya uhakiki na uthibitishaji wa taarifa ni muhimu kwa waandishi wa habari kwa kuwa yatawawezesha kuwa na uelewa wa kutambua na kuthibitisha taarifa hizo, ili kuwasaidia wananchi kupata taarifa sahihi zitakazowawezesha kufanya maamuzi sahihi.

Sauti ya Edward Chaina Afisa Programu Jamii Africa