Jamii FM

Watumishi TARI watakiwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma

16 May 2025, 11:19 am

Baadhi ya watumishi wa TARI nchini wakisikiliza kwa umakini hotoba ya mgeni rasmi (Picha Karimu Faida)

Watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kutoka kituo cha Naliendele na vituo vingine nchini wametakiwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao

Na Mwanahamisi Chikambu

Watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kutoka kituo cha Naliendele na vituo vingine nchini wametakiwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Bi. Judith Nguli, mnamo Mei 13, 2025, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa watumishi wa umma, yaliyofanyika katika kituo cha TARI Naliendele, mkoani Mtwara.

Bi. Nguli amesisitiza kuwa maadili ni msingi wa utendaji bora wa kazi, na amewahimiza wataalamu wa kilimo kutumia ujuzi wao kukuza mazao ya chakula kama mpunga, mbogamboga na mahindi ili kuinua kipato na ustawi wa wakulima nchini.

Sauti ya Judith Nguli Dc Mvomero
Mkuu wa wilaya ya Mvomero Bi Judith Nguli akizungumza na baadhi ya watumishi wa TARI katika ukumbi wa mikutano wa TARI-Naliendele(Picha na Karimu Faida)

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kituo cha TARI Naliendele, Bi. Geradina Mzena, amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea watumishi misingi imara ya maadili ambayo yatasaidia katika kufanya tafiti zenye tija na kutatua changamoto mbalimbali za wakulima.

Sauti ya Geradina Mzena mkurugenzi wa TARI Naliendele

Washiriki wa mafunzo hayo wameeleza kuwa yamekuwa ya manufaa makubwa kwao, kwani yamewakumbusha umuhimu wa kuwa waadilifu, kuwajibika, na kutoa huduma bora kwa wakulima na jamii kwa ujumla.

Sauti ya watumishi wa TARI Tanzania
Baadhi ya watumishi wa TARI nchini wakisikiliza kwa umakini hotoba ya mgeni rasmi (Picha Karimu Faida)