Jamii FM

Wavuvi waliopotea baharini Mtwara bado hawajaonekana

14 May 2024, 08:06 am

Vyombo vya uvuvi (Boti) zikiwa katika eneo la pwani la soko la Samaki Feri Mtwara (Picha na Musa Mtepa)

Boti hiyo ambayo ilikwenda baharini jioni ya tarehe 9/5/2024 kwa matarajio ya kurudi asubuhi  ya tarehe 10/5/2024  lakini hawakufanikiwa kurudi baada ya kupata hitilafu na walinipigia simu kuanzia saa kumi na moja hadi saa sita mchana wakaniambia mwenyekiti simu zetu zinaisha chaji kuanzia hapo hatukuwapata tena

Na Musa Mtepa

Boti ya uvuvi iliyobeba Wavuvi watatu wanaovua Bahari ya Hindi Mkoani Mtwara  inayohofia kupotea kwa kuzama Baharini wakati wakiwa katika shughuli za uvuvi hadi kufikia leo 13/5/2024 bado haijonekana .

Akizungumza na Jamii fm radio mwenyekiti wa jumuia ya Wavuvi Manispaa ya Mtwara Mikindani Mzee Sheha Shante amesema hadi kufikia leo tarehe 13/5/2024  wavuvi hao hawajaonekana na jitihada za kuwatafuta zikiwa zinaendelea ambapo Boti tatu za watafutaji zimeshafika katika maeneo ya kilwa  na Mafia katika utafutaji huo

Sauti ya 1 Sheha Shante Mwenyekiti wa jumuia ya wavuvi Manispaa ya Mtwara Mikindani

Hata hivyo Mwenyekiti huyo ameonesha kusikitika kutokuwepo kwa wadau wa Bahari na Serikali kuwepo kwa chombo cha uokozi kitakacho Saidia kuokoa kuliko kutegemea vya taasisi nyingine ambazo zinahitaji mchakato mrefu kuvipata vyombo hivyo.

Sauti ya 2 Sheha Shante Mwenyekiti wa jumuia ya wavuvi Manispaa ya Mtwara Mikindani

Mwenyekiti wa Soko la Feri Manispaa ya Mtwara Mikindani Mwinyi Mzaina amelishauri jeshi la zimamoto na uokoaji  Pamoja na serikali kujipanga vizuri  kwa upande wa Baharini kama walivyojipanga kwa upande wa nchikavu kwani anamini ya kuwa kama wangekuwa na vyombo vya uokoaji vya baharini wangefanikiwa kuwaokoa kwa wakati wavuvi hao.

Sauti ya Mwinyi Mzaina Mwenyekiti wa soko la feri Mtwara
Boti za uvuvi zikiandaliwa kuelekea Baharini kwa ajili ya uvuvi katika soko la Feri Mtwara (Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Mtwara zimeelezea hatua na jitihada zilizofanyika katika kuwaokoa wavuvi hao amabapo walifanikiwa kupata Boti ya polisi (Police Marine) kwa ajili ya kuwatafuta lakini hawakuweza Kwenda kwa wakati kutokana na changamoto ya Muda(usiku).

Sauti ya Taki Nguzo Kamishina Msaidizi Mwandamizi Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Mtwara

Wavuvi waliopotea ni Hashimu Faki,Hamisi Zahoro na Athumani Hamueji waliokuwa wanatumia Boti inayo julikana kama  Marua  ambao inasemekana wana asili ya visiwa vya Zanzibari.