Jamii FM

Kapela: Wanaume msiwabeze wanawake kwenye uongozi

12 July 2024, 09:42 am

Diwani wa kata ya Njengwa Mh Moza Salumu Kapela akiwa katika mahojiano maalumu na Musa Mtepa,Mwandishi wa habari wa Jamii fm radio Mtwara .

Changamoto kubwa aliyokutana nayo Bw Mustafa Chona wakati anampambania mkewe kuwa diwani wa kata ya Njengwa ni kwa baadhi ya wanaume kumdhihaki kuwa anapoteza muda wa kumpambania mkewe na kujirudisha nyuma kimaendeleo kwa kuuza baadhi ya mali na mifugo ili kumsaidia mke wake katika harakati za uongozi.

Na Musa Mtepa

Wanaume wameshauriwa kuwaandaa watoto wa kike na  kuwa mstari wa mbele katika kupigania na  kuhakikisha mwanamke anakuwa kiongozi  ili kuondoa dhana ya kuwa mwanamke hawezi kuwa kiongozi katika jamii.

Wito huo umetolewa na Moza Salumu Kapela diwani wa kata ya Njengwa wakati wa mahojiano maalum na Jamii fm Radio ambapo amesema kuwa nafasi aliyonayo hivi sasa ni kutokana na  juhudi kubwa zilizofanywa na mumewe na wakati mwingine amekuwa muhimizaji mkubwa katika kutekeleza majukumu yake hivyo ni wakati kwa wanaume wengine kuiga na kuwapa nguvu wanawake hasa wanapoonesha nia ya kuwa kiongozi.

Sauti ya 1 Moza Salumu kapela Diwani wa kata ya Njengwa Halmashauri yam ji Nanyamba Mtwara Dc

Aidha Mh Moza amesema kuwa kutokana na moyo na jitihada alizozionesha kwake wengi wanafikiri mume wake ni mfanyabiashara ila kiuhalisia ni mkulima tena ni mkulima wa hali ya chini.

Sauti ya 2 Moza Salumu kapela Diwani wa kata ya Njengwa Halmashauri yam ji Nanyamba Mtwara Dc

Kwa upande wake Mustafa Chona mume wa Moza Kapela diwani wa kata ya Njengwa amesema walikubaliana wote kwa Pamoja kupambania nafasi hiyo kwa kipindi kirefu kwa kuanzia katika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama huku malengo yao makubwa yakiwa siku moja kuwa Diwani wa kata ya Njengwa ili aweze kuwatatulia Wananchi kero zilizokuwa zinawakabiri.

Sauti ya 1Mustafa Chona mume wa Moza Kapela diwani wa kata ya Njengwa.
Mustafa Chona mume wa diwani wa kata ya Njengwa akiwa katika mahojiano na Musa Mtepa ,Mwandishi wa habari wa jamii fm radio juu ya jitihada alizozifanya hadi mke wake kuwa diwani wa kata hiyo.

Pamoja na hayo Mustafa Chona ametoa wito kwa wanaume wanaoamini Mwanamke hawezi kuwa kiongozi katika jamii ambapo amesema kuwa wanawake wanaweza kuwa kiongozi na kusimamia vizuri na wakati mwingine zaidi ya mwanaume .

Sauti ya 2Mustafa Chona Mume wa Moza Kapela diwani wa kata ya Njengwa

Kata ya Njengwa ni mara ya kwanza inakuwa na diwani mwanamke ambapo baada ya kuingia madaraka Mheshimiwa Moza Kapela amefanikisha upatikanaji wa uhakika wa huduma ya umeme,maji ,Barabara na miundombinu mbalimbali ya madarasa kwa shule za Msingi na Sekondari pamoja na Zahanati hali ambayo ilikuwa tofauti na hapo awali kwa viongozi wengine waliopita kwa kipindi cha Nyuma.