Jamii FM

TANECU yauza korosho tani 3,857 kwa  Tsh 4,120

11 October 2024, 15:50 pm

Mnada wa leo wameshindana makampuni 37 na korosho zote zilizouzwa zimenunuliwa na makampuni 10 hivyo makampuni 27 yamekosa korosho maana yake ni kwamba kunauhitaji wa korosho duniani na beii hii  ni kutokana  dunia ina uhitaji mkubwa wa korosho karanga na kutokana na hilo italeta hamasa kwa wakulima kuhudumia mashamba yao vizuri.

Na Grace Hamisi

Chama kikuu cha ushirika kinachohudumia Tandahimba na Newala (TANECU) kimefanikiwa kuuza tani 3,857 za korosho katika mnada wa kwanza uliofanyika leo, tarehe 11 Oktoba 2024, katika wilaya ya Newala, mkoani Mtwara. Ambapo bei ya juu kupitia Mnada huo ni Tsh. 4,120 na Tsh. 4,035 bei ya chini

Akizungumza katika ufunguzi wa mnada huo, Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, amesisitiza umuhimu wa wakulima kuhakikisha wanazalisha korosho zenye ubora ili waweze kupata bei nzuri inayowaridhisha.

Sauti ya Kanali Patrick Sawala mkuu wa mkoa wa Mtwara
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala akizungumza na wakulima baada ya mnada huo kufanyika mjini Newala

Kwa upande mwingine, Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho, Fransis Alfred, ameeleza kuwa hadi jana, kampuni 45 zilikuwa zimekidhi vigezo na kupata leseni ya kununua korosho.

Sauti ya Francis Alfred Mkurugenzi wa bodi ya korosho Tanzania(CBT)
Francis Alfred akizungumzia hali ya soko la korosho Duniani baada ya mnada wa zao hilo kufanyika hii leo

Bi. Rukia Silimu, mkulima kutoka kijiji cha Mwangaza, ameeleza furaha yake kuhusu bei hii, akisema kuwa hakuweza kutarajia mabadiliko mazuri ikilinganishwa na miaka iliyopita ambayo ilikuwa na changamoto nyingi.

Sauti ya Rukia Mwangaza mkulima wa zao la korosho wilayani Tandahimba
Baadhi ya viongozi wa vyama vya Ushirika na wakulima wakifuatilia mwenendo wa soko mtandaoni kupitia mnada wa korosho uliofanyika mjini Newala hii leo

Kwa ujumla, habari hii inaonyesha mwelekeo chanya katika soko la korosho, inatoa matumaini kwa wakulima wa zao hilo.