Jamii FM

Wakulima  washauriwa kuzingatia ubora wa ufuta ukiwa shambani

11 May 2024, 14:10 pm

Dr Fortunus Kapinga mkurugenzi wa (TARI)Naliendele akizungumza na Waandishi wa habari alipotembelewa na Wanafunzi wa chuo cha mafunzo ya kilimo (MATI) Mtwara

Kutokana na mnada uliofanyika nuzi mkoani Songwe unatoa picha kuwa hali ya bei ya ufuta kwa mwaka huu inaweza kuwa mzuri na itasaidia kuwaongezea kipato wa kulima lakini pia kuliingizia fedha taifa lakini pia inaweza kuwa kichocheo  kwa vijana kuijiingiza kwenye kilimo

Na Musa Mtepa

Wakulima wa ufuta wameaswa kuzingatia mambo ya msingi kabla na  baada ya kuvuna ili waweze kupata soko zuri la zao hilo.

Wito huo umetolewa tarehe 10/5/2024 na mkurugenzi wa Taasisi ya utafiti wa kilimo ( TARI) Naliendele Dr Fortunus Kapinga  alipotembelewa na Wanafunzi wa chuo cha mafunzo ya kilimo Mtwara (MATI) ambapo amesema kuwa wakulima wanatakiwa kuangalia umuhimu wa ubora wa ufuta  wenyewe kwa kuanzia shambani hadi kwenda kwenye soko.

Sauti ya 1 Dr Kapinga mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa kilimo (TARI) Naliendele

Aidha Dr Kapinga amesistiza ubora pia unaweza kuharibika wakati wa kupeleka Gharani kwa kutozingatia utaratibu sahihi uwekaji kwenye magunia na kutopepetwa vizuri.

Sauti ya 2 Dr Kapinga mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa kilimo (TARI) Naliendele

Kwa upande wake mratibu wa mpango wa utafiti wa ufuta kitaifa na mtafifiti wa zao la ufuta kutoka taasisi ya utafiti wa kilimo (TARI) Naliendele Joseph Mzunda amesema  kuwa kutokana na mnada uliofanyika hivi karibuni mkoani Songwe bei ya ufuta kwa  kilo moja imeuzwa shilingi elfu 4,500  na kusema kuwa kunauwezekano wa bei kuendelea kupanda .

Joseph Mzunda mratibu wa mpango wa utafiti wa ufuta kitaifa na mtafifiti wa zao la ufuta kutoka taasisi ya utafiti wa kilimo (TARI) Naliendele akizungumzia hali ya soko la ufuta kwa kipindi hiki.

Sambamba na hilo amewaomba wakulima zao hilo kuuza katika mfumo unaoeleweka pamoja na kufuata taratibu sahihi za uvunaji na utunzaji wake kabla ya kupeleka sokoni.

Dr Fortunus Kapinga mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa kilimo ( TARI) Naliendele akionesha ufuta unaotakiwa usio takiwa na unao takiwa kuvunwa ukiwa shambani.