Jamii FM

Wananchi kuchangia 2,000 kumleta mganga wa asili kijijini

10 December 2025, 21:16 pm

Wananchi wa kitongoji cha Nunu wakiwa katika mkutano wa kujadili changamoto ya mlipuko wa moyo (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Kitongoji cha Nunu, Msakala, wameamua kuchangia shilingi 2,000 kwa kila nyumba ili kumleta mganga wa jadi baada ya hofu ya “mlipuko wa ugonjwa wa moyo.” suluhisho

Na Musa Mtepa

Katika hali ya kushangaza, wananchi wa kitongoji cha Nunu kilichopo katika Kijiji cha Msakala, Kata ya Ziwani, Halmashauri ya Mtwara vijijini wamekubaliana kuchangia shilingi 2,000 kwa kila nyumba ili kufanikisha kuletwa kwa mganga wa asili (Jadi) atakayesaidia kutafuta na kutatua changamoto ya wananchi kukumbwa na kile wanachokieleza kuwa ni “mlipuko wa ugonjwa wa moyo.”

Wakizungumza katika mkutano wa kitongoji ulioitishwa Desemba 10, 2025 kwa lengo la kujadili namna ya kukabiliana na tatizo hilo, wananchi wamesema kuwa  hali hiyo imeleta taharuki kubwa na kuchochewa na imani za kishirikina kwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo.

Sauti ya Wananchi wa kitongoji cha Nunu

Cornel Caspari, ambaye ni muhanga na mkazi wa kitongoji hicho, amesema kijana wake alipokumbwa na tatizo hilo alianza kuhisi maumivu ya mwili na baadaye kupata matatizo ya moyo yaliyomsababisha kuanguka chini na baadae kuinuka na kuanza kukimbia kusikojulikana huku akitamka majina ya watu wasiojulikana ( kuweweseka).

Sauti ya Cornel Caspari Muhanga wa tukio

Naye Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nunu, Bw. Matias Poolu, amesema ukubwa wa changamoto hiyo ndiyo uliowalazimu kuitisha mkutano wa wananchi ili kujadili na kutafuta suluhisho, ambapo kwa kauli moja walikubaliana kuchangia shilingi 2,000 kwa kila nyumba.

Sauti ya Matias Pool Mwenyekiti wa kitongoji cha Nunu

Hamisi Salumu Namngwangula, Mwenyekiti wa kijiji cha Msakala ambacho kinahudumia Kitongoji cha Nunu, amekiri kuwepo kwa matukio ya wananchi kukumbwa na changamoto hiyo na kupongeza hatua ya wananchi kuitisha mkutano ili kujadiliana na kufikia muafaka.

Sauti ya Hamisi Namngwangula Mwenyekiti wa kijiji cha Msakala