Jamii FM

Jamii yahimizwa kuepuka hisia katika kutatua migogoro

9 December 2025, 12:25 pm

Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka shirika la TASA Hamisi Mwinshehe akiwa katika studio za Jamii fm Mtwara

Afisa wa TASA, imeitaka  jamii kutenga muda wa kufikiria na kutoa maamuzi sahihi katika kutatua migogoro, ikisisitiza kuepuka hisia na kutoegemea upande wowote

Na Musa Mtepa

Jamii imetakiwa kutenga muda wa kufikiria, kuchakata na kutoa maamuzi sahihi katika kutatua migogoro inayowakabili katika maeneo yao.

Hayo yamesemwa na Afisa Tathmini na ufuatiliaji kutoka shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Safety Alliance (TASA) linalofanya kazi katika Manispaa ya Mtwara–Mikindani, Hamisi Rashidi Mwinshekhe, kupitia kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na kituo cha redio cha Jamii FM Mtwara.

Amesema kuwa mgogoro ni hali ya kuwepo kwa mivutano ya kimawazo au kimtazamo, hivyo ni muhimu jamii kutenga muda wa kutosha wakati wa mchakato wa utatuzi ili kuhakikisha kila upande unaridhika na maamuzi yatakayofikiwa.

Sauti ya 1: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Aidha, Mwinshekhe amesema kuwa kumekuwa na sababu mbalimbali zinazosababisha kuibuka kwa migogoro katika jamii, ambazo kwa namna moja au nyingine ni muhimu kuepukika ili kujenga jamii imara na yenye amani.

Sauti ya 2: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Ameongeza kuwa kuna mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kutatua migogoro, ikiwemo kuepuka matumizi ya hisia, kuonesha huruma, pamoja na kutoegemea upande wowote katika mgogoro unaoendelea.

Sauti ya 3: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Shirika la TASA kwa sasa linatekeleza mradi wa “Amani Yetu, Kesho Yetu” katika kata tano za Halmashauri ya Mtwara Vijijini, ambazo ni Nalingu, Madimba, Msimbati, Tangazo na Mahurunga.

Mradi huu unalenga kuelimisha jamii, hususan vijana, kuhusu athari za uvunjifu wa amani na umuhimu wa kudumisha utulivu katika maeneo yao.