Jamii FM

NEMC Kanda ya Kusini yashiriki zoezi la upandaji wa mikoko Namela

5 June 2024, 16:47 pm

Meneja wa NEMC kanda ya kusini Mhandisi Boniphace Guni akiongoza zoezi la upandaji miti aina ya mikoko eneo la Kigongo katika kijiji cha Namela kata ya Msangamkuu wilayani Mtwara(Picha na Musa Musa)

Kati ya miti ambayo inafyonza hewa chafu kwa uwingi na kwa haraka ni mikoko hivyo kitendo cha kupanda katika eneo la kigongo ni katika kuendeleza harakati za kupunguza hewa chafu na ni fursa kwa maeneo mengine ya pwani ya kusini kuwa na utaratibu wa upandaji wa miti hii

Na Musa Mtepa

Meneja wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kusini  Mhandisi Boniphace Guni   Juni 4, 2024 ameshiriki zoezi la upandaji wa mikoko  eneo la Kigongo katika kijiji cha Namela  kata ya Msangamkuu wilaya na mkoani Mtwara.

Zoezi hilo lililohusisha vijana wa Madrasat Sabilia tawi la Msangamkuu,umoja wa usimamizi wa rasilimali za bahari (BMU) Namela Pamoja na viongozi wa serikali ya Kijiji

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji kukamilika meneja wa NEMC kanda ya kusini  Mhandisi Boniphace Guni amefurahishwa na jitihada zilizofanywa na BMU Kijiji cha Namela kwa kitendo cha kutunza mazingira  eneo la kigongo katika hali ya asili  huku  akiiomba jamii   kushirikisha vijana ili baadae waweze kuwa mabalozi wazuri katika utunzaji wa mazingira.

Sauti ya 1 Meneja wa NEMC kanda ya kusini Mhandisi Boniphace Guni
Meneja wa NEMC kanda ya Kusini Mhandisi Boniphace Guni akielezea umuhimu wa upandaji wa miti ya mikoko katika utunzaji wa Mazingira(Picha na Musa Mtepa)

Aidha Mhandisi Guni amememuomba  mtendaji wa Kijiji cha Namela Pamoja na viongozi wa BMU kuhakikisha  mikoko iliyopandwa  katika eneo hilo inalindwa na kutunza ili jitihada zilizofanyika zisipotee bure.

Sauti ya 2 meneja wa NEMC kanda ya Mhandisi Boniphace Guni

Kwa upande wake  Kulwa Issa Saidi katibu wa jumuia ya umoja wa usimamizi wa rasilimali za Bahari (BMU) kata ya Msangamkuu amesema katika kuahakikisha eneo la pwani linakuwa safi  wamekuwa wakifanya usafi katika eneo la fukwe,kulima kilimo cha Mwani Pamoja na kupanda mikoko ikiwa njia mojawapo ya kutunza mazingira.

Sauti ya  kulwa Issa Saidi katika wa umoja wa usimamizi wa Pwani kata ya Msangamkuu
Katibu wa jumuia ya umoja wa usimamizi wa rasilimali za bahari Kulwa Issa Saidi akizungumzia namna wanavyohakikisha wanaweka safi mazingira ya bahari kwa kata ya msangamkuu(Picha na Musa Mtepa)

Naye Ostadhi Mubaraka Juma kutoka  Madrasat Sabilia amesema kuwa hata kwa viongozi watukufa wa dini wameelezea umuhimu wa kutunza mazingira hivyo wao kama viongozi wa kiimani watahakikisha wanashirikiana na vijana katika kulinda na kutunza mazingira kama maandiko yanavyoelezea.

Sauti ya Ostadhi Mubaraka Juma kutoka Al madrasat Sabilia tawi la msangamkuu Mtwara vijijini
Eneo la kigongo lililopo katika kijiji cha Namela kata ya Msangamkuu linalopandwa miti aina ya mikoko ili kurejesha uoto wake wa asili ikiwa njia ya kuhifadhi na kutunza mazingira ya bahari(picha na Musa Mtepa)