Jamii FM

Mashabiki wa Simba Mtwara wafanya usafi, dua kuwaombea wachezaji

3 August 2024, 18:02 pm

Baadhi ya mashabiki wa Simba walikusanyika katika kijiji cha Kawawa wakiowaombea dua wachezaji na viongozi wa timu katika kuelekea msimu mpya wa mashindano (Picha na Musa Mtepa)

Matarajio makubwa kwa mashabiki wa timu ya Simba ni kuona inafanya vizuri katika mashaindano mbalimbali itakayoshiriki timu hiyo kwa msimu wa 2024/2025 na hii ni kutokana na kufanya usajili unaotoa mategemeo makubwa kwa mashabiki wao.

Na Musa Mtepa

Mashabiki wa timu ya simba kutoka Kijiji cha Kawawa kata ya Mkunwa wilaya ya Mtwara  mkoani Mtwara wamesheherekea siku ya Simba(Simba day) kwa kufanya usafi katika Shule ya Msingi Kawawa,Zahanati ya Kawawa ,Msikiti mkuu wa Kawawa Pamoja na kuwafanyia Dua Wachezaji ,Viongozi na mashabiki katika kuelekea msimu mpya wa Mashindanzo.

Akizungumza na jamii fm redio leo August 3,2024 Mwenyekiti wa mashabiki hao Mohamedi Dadi Nakandu amesema katika kusheherekea siku hiyo wamefanya usafi katika maeneo mbalimbali ya kijamii huku akisema kuwa hiyo ni kuonesha simba kweli ni nguvu na ndio maana wamefanya hayoi yote.

Sauti ya Mohamedi Dadi Mwenyekiti wa mashabiki wa Simba Kijiji cha Kawawa Mtwara DC.
Mashabiki wa Simba kutoka kijiji cha Kawawa Mtwara Vijijini wakiwa katika mkutano baada ya kumaliza kufanya usafi (Picha na Musa Mtepa)

Naye Mwalimu Lyuma msemaji wa mashabiki wa Simba Kijiji cha Kawawa amesema kuwa wameamua kufanya matukio hayo wakiwa kama sehemu ya jamii ikiwa katika kurudisha fadhila kwa kuwaunga mkono yale yanayofanywa na viongozi wa kitaifa katika kusheherekea siku ya Simba day.

Sauti ya Mwalimu lyuma msemaji wa mashabiki wa simba Kijiji cha kawawa

Himidi Bakari Namakanya Mwenyekiti wa Kijiji cha Kawawa amewashukuru mashabiki wa Simba kwa kitendo cha kufanya usafi na kutoa msaada wa fedha  katika maeneo ya kijamii  huku akiwataka mashabiki wat imu nyingine kuiga kitendo hicho.

Sauti ya Himidi Bakari Namakanya Mwenyekiti wa Kijiji cha kawawa Mtwara DC

Akizungumza kwa niaba ya taasisi zilizofanyiwa usafi kiongozi wa Msikiti mkuu wa Kijiji cha Kawawa Shekhe Hamisi Mfaume Palangadau  amesema kupitia maandiko mwenyezi mungu ameelezea umuhimu wa kufanya usafi katika mazingira yanayo mzunguka Binadamu hivyo kwa kitendo kilichofanywa na mashabiki hao ni sehemu ya kutekeleza maandiko hayo.

Sauti ya Shekhe Hamisi Mfaume Palangadau kiongozi wa dini ya kiislamu kutoka Kijiji cha Kawawa.
Mashabiki wa Simba kijiji cha Kawawa wakijiandalio Chakula baada ya kufanya usafi pamoja na Dua ya kuwaombea wachezaji na viongozi wa timu hiyo(Picha na Musa Mtepa)

Baada ya kufanya usafi mashabiki hao walifanya dua ya kuwaombea Wachezaji wa Simba ,Viongozi na mashabiki wa timu hiyo iliyoenda sambamba na viburudisho mbalimbali vikiwemo chakula na Vinywaji .