Jamii FM

Tamasha la Red Scopion La vunja rekodi mkoani Mtwara

1 September 2024, 11:06 am

Mashabiki wa timu ya Red scopion kutoka kijiji cha Mgao wakiwa wameshikiria Bendera yenye nembo ya timu hiyo (picha na Musa Mtepa)

“Malengo yetu sisi ni kutambulika na chama cha soka mkoani Mtwara (MTWAREFA) pamoja na kuwa timu kubwa itakayo kuwa inashiriki mashindano mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Mtwara lakini pia kuwa timu ya kukuza na kuuza vipaji “

Na Musa Mtepa

Timu ya Red Scopion kutoka Kijiji cha Mgao August 31,2024 imeadhimisha kilele cha siku ya timu hiyo (RED SCOPION DAY) iliyohusisha utambulisho wa Wachezaji watakao tumika katika msimu wa mashindano ya  2024/25 .

Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi katibu msaidizi wa timu hiyo Omari Hamisi amesema malengo ya timu ni Pamoja na kujisajili katika chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mtwara (MTWAREFA ) .

Aidha Omari Hamisi amesema Pamoja na mafanikio hayo wamekuwa na changamoto mbalimbali zilinazo wakabili ikiwa Pamoja na ukosefu wa fedha za kufanyia usajili na upungufu wa vifaa vya michezo .

Sauti ya Omari Hamisi katibu msaidi wat imu ya Red scopion kutoka Kijiji cha Mgao.
Viongozi wa timu ya Red scopion wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa tamasha la timu hiyo(Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake mgeni rasmi wa tamasha hilo mdau wa michezo ambe pia ni Diwani wa kata ya Mayanga Mhe. Arif Premji amefurahishwa na kitendo cha kualikwa katika tamasha hilo huku akitatua changamoto ya jezi na fedha za usajili zilizokuwa zinaikabili timu hiyo ili iweze kutambulika na chama cha mpira wa miguu mkoani Mtwara (MTWAREFA).

Sauti ya Arif Premji Mdau wa michezo wilayani Mtwara ambae pia ni diwani wa kata ya Mayanga.
Mdau wa michezo ambae pia diwani wa kata ya Mayanga wilayani Mtwara Arif Premji Mgeni rasmi akizungumza mbele ya wapenzi na mashabiki wa timu ya red scopion (Picha na Musa Mtepa)

Juma Nangomwa mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Mtwara amesema uwepo wa matamasha ya kimichezo inasaidia kuleta hamasa kwa jamii kujiingiza katika michezo  na kusistiza hamasa hizo kutoishia kwenye matamasha pekee .

Sauti ya Juma Nangomwa mwenyekiti wa chama cha Mpira wa miguu wilaya ya Mtwara.

Akielezea malengo ya tamasha la Red Scopion na timu kwa ujumla mwenyekiti wa timu hiyo Selemani Mzee Salumu amesema kuwa malengo ni kuwa timu kubwa itakayoshiriki mashindano mbalimbali Pamoja na kukuza na kuuza vipaji vya wachezaji wao.

Sauti ya Selemani Mzee Mwenyekiti wat imu ya Red Scopion ya Kijiji cha Mgao

Nao Mashabiki  wameonesha kufurahia tamasha hilo na kuhitaji kuwa na mwendelezo wa uwepo wa tamasha hilo kwani kwao limekuwa sehemu ya sikukuu.

Sauti ya Mashabiki wa red scopion kutoka Kijiji cha Mgao.
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza kwenye tamasha la Red scopion wakifuatilia Burudani ya muziki katika tamasha hilo(Picha na Musa Mtepa)

Tamasha la Red scopion limefanyika jana August 31,2024 katika Kijiji cha Mgao kilichopo kata ya Naumbu Halmashauri ya Mtwara vijijini mkoani Mtwara ambapo katika tamasha hilo kulikuwepo na  burudani mbalimbali kama vile Muziki kutoka Msanii LastBorn kutoka Kijiji cha Mgao aliyetambulisha wimbo wake mpya kwenye tamasha hilo,Dogo Chidy msanii anae tamba na wimbo wa Usijali ,Wachezaji Muziki kutoka katika Kijiji cha Mgao na utambulisho wa wachezaji watakao shiriki mashindano mbalimbali katika msimu wa 2024/25.

Aidha katika kuhitimisha tamasha hilo kulifanyika mchezo wa mpira wa miguu katika timu mwenyeji ya Red scopion fc na Jordan fc kutoka katika Kijiji cha Mnima ambapo mwenyeji alikubali kichapo cha goli moja bila.