Mpanda FM

Recent posts

4 March 2023, 1:54 pm

Mgogoro wa wachimbaji Dirifu, DC ataka subira

MPANDAMkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amewataka Wananchi na wachimbaji wa madini wa kijiji cha Dirifu kuwa na subira na kuishi kwa amani kufuatia mgogoro unaoendelea katika kijiji hicho. Akitoa maelekezo hayo kutoka ofisi ya mkuu wa wilaya ya…

22 February 2023, 6:55 pm

Wananchi Tanganyika Waaswa Kuchangia Miundombinu ya Elimu

TANGANYIKA. Wananchi wa halmashauri ya Tanganyika wametakiwa kuiunga mkono serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu ili kumsaidia mtoto wa kike kupata elimu bora. Wakizungumza na Mpanda redio fm baadhi ya wananchi wametaja kuwa ubovu wa miundombinu shuleni ni moja ya…

22 February 2023, 6:42 pm

Ajira kwa Watoto Bado Changamoto Katavi

KATAVI Wananchi Halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelaani wazazi wanaoruhusu watoto wadogo kufanya biashara muda ambao walitakiwa wawe shule. Wakizungumza na kituo hiki wananchi hao wamesema kuwa vitendo hivyo vinaathiri saikolojia za watoto na kuwapotezea malengo yao ya…

22 February 2023, 6:37 pm

Elimu ya Ukimwi kwa Mama na Mtoto

MPANDA Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametoa maoni yao jinsi mama aliye na maambukizi ya virusi vya ukimwi anavyoweza kumlinda mwanae asipate maambukizi hayo. Wakizungumza na mpanda radio fm wananchi hao wamesema kuwa mama anatakiwa kwenda…

22 February 2023, 6:33 pm

Wananchi Waaswa Kuchukua Tahadhari ya Surua

KATAVI Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa surua ulioibuka katika halmashauri ya mpimbwe mkoani katavi. Hayo yamesemwa na Dr solomon solomoni wakati akizungumza na Mpanda redio fm na kuainisha kuwa mlipuko wa surua unaathiri zaidi watoto chini ya…

22 February 2023, 6:28 pm

Sheria ya Mita 60 Bado Changamoto

MPANDA Utekelezaji wa sheria ya kutofanya shughuli za kibinaadamu ndani ya mita 60 kutoka mtoni umekuwa bado una changamoto kwa wakazi wanaoishi karibu na maeneo ya mito licha ya msisitizo kuhusu sheria hiyo. Baadhi ya wakazi wanaoishi kuzunguka mto Mpanda…

22 February 2023, 6:24 pm

Diwani Magamba Alia na Tanesco

MPANDA Diwani wa Kata ya Magamba Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Fortunatus Maiko ameliomba Shirika La Umeme [Tanesco] kutoa ufafanuzi kuhusiana na Matumizi ya unit za umeme ili kuondoa mkanganyiko unaoendelea kuonekana kwa ya wananchi. Ameyasema hayo alipokuwa kwenye baraza…

22 February 2023, 6:18 pm

Mtapenda Yaendeleza Kampeni ya Upandaji Miti

NSIMBO Katika kuunga mkono Kampeni ya serikali ya upandaji wa miti kata ya Mtapenda Halmashauri Ya Nsimbo Mkoani Katavi imeanza zoezi la upandaji wa miti katika vijiji vyake kwa lengo la kuendelea kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Wakizungumza na…

16 February 2023, 6:10 am

Umaskini Wachangia Elimu Kuwa Chini Katavi

KATAVIUmaskini, uelewa mdogo wa Wazazi na Walezi ni miongoni mwa sababu zinazoelezwa na baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Mpanda kupelekea Elimu kuwa Chini katika mkoa wa Katavi. Wakizungumza na Mpanda Radio wakati wakitoa maoni kuhusu ubora wa elimu Wananchi…

16 February 2023, 6:06 am

Elimu Itolewe Juu ya Ugonjwa wa KifuaKikuu

MPANDA Serikali Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imetakiwa kuongeza juhudi za utoaji wa elimu ya ugonjwa wa Kifua Kikuu ili kuwapatia wananchi uelewa juu ya ugonjwa huo Hayo yamebainishwa na wananchi wa Manispaa ya Mpanda wakati wakizungumza na Mpanda Radio…

Kuhusu Mpanda Radio

Umiliki wa redio
Mpanda Radio FM inamilikiwa na kampuni iliyosajiliwa iitwayo Mpanda radio FM Limited na cheti cha usajili namba 78298 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpanda Radio FM pia imesajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania TCRA, Wizara ya Viwanda na biashara; ama tunatambuliwa na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania TCCIA na Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kama Mlipa Ushuru, tuna Namba ya Kitambulisho cha Mlipa kodi 115-577-239 na tumepewa nambari ya usajili ya VAT 40-015708 kwa Biashara iliyoko hoteli ya Mpanda, eneo la eneo. nambari G, nambari ya kuzuia 35.

Dira
Kuwa jamii thabiti yenye afya bora, elimu, umoja na maendeleo endelevu, inayotambua wajibu na haki.

Dhamira
Kushirikisha jamii katika kuandaa vipindi, habari na uendeshaji wa redio kwa kuzingatia taaluma. Kuwa jukwaa la mijadala inayochochea mabadiliko chanya ya fikra, usawa wa jinsia, sheria na utawala bora, uwajibikaji, ushindani wa maendeleo, utamaduni na ulinzi wa rasilimali.

Uongozi
Mpanda Radio FM ina mlolongo mzuri wa uongozi na inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi. Tuna wakurugenzi watatu kwa hisa na kuajiriwa; pia tuna uongozi wa uzalishaji na uuzaji.