Mpanda FM

Recent posts

27 April 2023, 8:19 am

Wananchi 53 Mpanda Wanufaika na Mafunzo ya Ujasiriamali

MPANDA Jumla ya wananchi 53 manispaa ya Mpanda mkoani katavi ikiwamo wanawake pamoja na vijana wamenufaika na mafunzo ya ujasiliamali yaliyowezeshwa na Diwani wa viti maalumu kata ya majengo kupitia chama cha mapinduzi CCM lengo likiwa ni kuwapa ujuzi na…

22 April 2023, 9:45 am

Buswelu: Jipangeni Kukusanya Mapato Yanayopotea

TANGANYIKA Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu ametoa maelekezo kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Tanganyika kuangalia namna bora ya ukusanyaji wa mapato katika kipindi hiki cha mavuno. Maelekezo hayo ameyatoa wakati wa kikao cha baraza la madiwani wilaya ya…

22 April 2023, 9:38 am

Ulinzi Waimarishwa Sikukuu za Eid El Fitr

KATAVI Katika kuelekea sikukuu ya Eid El Fitri Jeshi la polisi mkoa wa Katavi limepanga kuimarisha ulinzi ili kupunguza uvunjifu wa sheria kipindi cha sikukuu. Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Katavi Ali Makame Hamad…

22 April 2023, 9:33 am

Ukosefu wa Maji Safi na Salama, Kilio Itenka

KATAVI Kufuatia changamoto ya magonjwa ya Tumbo na minyoo jamii imetakiwa kuzingatia kanuni za afya ili kuondokana na magonjwa hayo kwa baadhi ya wakazi wa Itenka Halmashauri ya Nsimbo mkoani Katavi. Hayo yamejiri mara baada ya wakazi wa Intenka halmashauri…

22 April 2023, 9:28 am

Wananchi Waaswa Kutumia Vituo vy Afya.

MPANDA Wananchi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuacha mila potofu ya kufuata huduma za matibabu kwa waganga wa kienyeji badala yake wajenge tabia ya kuvitumia vituo vya kutolea huduma za afya vinavyojengwa na serikali katika maeneo yao . Wameyasema…

18 April 2023, 9:40 pm

Walimu Mlele Wahakikishiwa Mazingira Rafiki

MLELE Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga amewahakikisha Walimu mazingira rafiki ya uendaji kazi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao waliyopewa na serikali. Mwanga ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha Wadau wa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Mlele…

18 April 2023, 9:35 pm

Mmoja Afariki kwa Kuangukiwa na Ukuta Shanwe

MPANDA Mtu Mmoja aliyefahamika kwa jina la Elizabeti Fabiano mwenye umri wa mika 29 mkazi wa Mtaa wa shanwe Manispaa ya Mpanda mkoa wa katavi amefariki Dunia Kwa kuangukiwa na nyumba Akizungumzia tukio Hilo mama mzazi wa marehemu Khadija Eneliko…

18 April 2023, 9:26 pm

Wazazi na Walezi Wametakiwa Kuwapa Watoto wao Elimu

MPANDA Wazazi na Walezi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuwapa kipaumbele watoto katika kupata elimu ili waweze kutimiza ndoto zao. Akizungumza katika hafla ya kutunukiwa udaktari kutoka chuo cha all nation christian church Askofu Laban Ndimubenya amewataka wazazi na…

18 April 2023, 9:20 pm

Mlele Yapongezwa kwa Utekelezaji wa Miradi ya Serikali

MLELE Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mlele Wolfgang Mizengo Pinda amepongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Kwa utekelezaji wa Miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kutokana na fedha za Serikali Kuu na usimamizi mzuri wa miradi hiyo. Pinda ametoa pongezi katika ziara…

Kuhusu Mpanda Radio

Umiliki wa redio
Mpanda Radio FM inamilikiwa na kampuni iliyosajiliwa iitwayo Mpanda radio FM Limited na cheti cha usajili namba 78298 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpanda Radio FM pia imesajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania TCRA, Wizara ya Viwanda na biashara; ama tunatambuliwa na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania TCCIA na Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kama Mlipa Ushuru, tuna Namba ya Kitambulisho cha Mlipa kodi 115-577-239 na tumepewa nambari ya usajili ya VAT 40-015708 kwa Biashara iliyoko hoteli ya Mpanda, eneo la eneo. nambari G, nambari ya kuzuia 35.

Dira
Kuwa jamii thabiti yenye afya bora, elimu, umoja na maendeleo endelevu, inayotambua wajibu na haki.

Dhamira
Kushirikisha jamii katika kuandaa vipindi, habari na uendeshaji wa redio kwa kuzingatia taaluma. Kuwa jukwaa la mijadala inayochochea mabadiliko chanya ya fikra, usawa wa jinsia, sheria na utawala bora, uwajibikaji, ushindani wa maendeleo, utamaduni na ulinzi wa rasilimali.

Uongozi
Mpanda Radio FM ina mlolongo mzuri wa uongozi na inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi. Tuna wakurugenzi watatu kwa hisa na kuajiriwa; pia tuna uongozi wa uzalishaji na uuzaji.