Mpanda FM
Mpanda FM
26 March 2026, 6:11 pm

“Biashara imekuwa ngumu”
Na John Benjamin
Baadhi ya wananchi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia kupanda kiholela bei ya nyama ya ng’ombe kutoka shilingi 10,000 hadi shilingi 12,000.
Wakizungumza na Mpanda Redio FM kwa nyakati tofauti wamesema kuwa kupanda kwa bei ya kitowewo hicho imewafanya kushindwa kumudu gharama na kuiomba serikali kuingilia kati swala hilo ili kuhakikisha bei inashuka na kuendana na hali ya maisha ya wananchi wa kawaida.
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wa bucha za nyama manispaa ya Mpanda wamesema kuwa kasi ya wanunuzi imepungua ukilinganisha na awali ambapo ameleeza kuwa hali hiyo imekuwa ikiwagharimu ambapo imekuwa ikisababisha kukaa kwa muda mrefu buchani.
Mwenyekiti wachinjaji mkoa wa Katavi Fadhili Makolokolo amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo amesema kuwa kupanda kwa bei ya nyama imesababishwa na kupanda kwa bei ya mifugo haswa Ngombe na hilo limesababishwa na uwepo wa wimbi la wanunuzi kutoka nje ya nchi.
Aidha Makolokolo ameiomba serikali kusimamia vyema wanunuzi wanaotoka nje ya nchi kuhakikisha wanafata sheria pindi wanapoingia nchi kununua mifugo.