Mpanda FM
Mpanda FM
20 March 2026, 5:55 pm

“Ni vyema kurudisha shukrani kwa mwenyezi Mungu kwa kuyafanya matendo hayo ya huruma “
Na Anna Milanzi- Katavi
Waganga wa tiba asili na tiba mbadala mkoa wa Katavi wamefanya matendo ya huruma kwa kuwatembelea watoto yatima na mama mjane anayeuguza mtoto wake.
Akizungumza kwa niaba ya waganga wa tiba asili Mwenyekiti wa tiba asili na tiba mbadala mkoa wa Katavi Gadius Luviga amesema wameona ni vyema kurudisha shukrani kwa mwenyezi Mungu kwa kuyafanya matendo hayo ya huruma .
Akitoa shukrani mara baada ya kupatiwa kiasi cha fedha cha Tshs laki moja mama anayeuguza mtoto mkazi wa mtaa wa Mpanda hotel amesema kiasi hicho cha fedha kimesaidia kupunguza kiasi cha fedha kinachohitajika katika matibabu ya mtoto wake.
Aidha wametembelea katika kituo cha kulelea watoto cha Yohana Paulo wa pili kilichopo manispaa ya Mpanda ambapo afisa ustawi mlezi wa kituo hicho ameeleza kuwa wamekuwa wakiwalea watoto waliopoteza wazazi wote wawili na hawana msaada,watoto waliotelekezwa,watoto ambao wazazi wao wanachangamoto ya afya ya akili pamoja na watoto wanaopitia ukatili .
Waganga wa tiba asili mkoa wa Katavi walipotembelea katika kituo hicho cha kulelea watoto yatima wametoa kiasi cha Tshs laki mbili fedha ambayo itasaidia katika mahitaji ya watoto na kuwaomba watu wengine kuendelea kuwatembelea watoto hao