Mpanda FM

RC Katavi asikiliza kero za wananchi

11 March 2026, 4:58 pm

Baadhi ya viongozi wakiwa kwenye kikao na wananchi. Picha na Leah Kamala

“Kila taasisi ipande miti”

Na Leah Kamala

Wananchi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameelezea kero mbalimbali zinazowakabili katika maeneo yao, na kumuomba mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kuzifanyia kazi ili kuboresha maisha yao.

Kero hizo ziliwasilishwa na wananchi katika kliniki ya kusikiliza kero, iliyohudhuria na mkuu wa mkoa wa Katavi, pamoja na viongozi wengine na mkoa, katika ukumbi wa manispaa.

Sauti za wananchi

Akizungumza wakati wa kusikiliza na kupokea kero mbalimbali za wananchi, mkuu wa mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko amesema kuwa changamoto zinazowakumba wananchi zinaendelea kupatiwa ufumbuzi, huku akisisitiza kufanya usafi ndani ya saa72, pamoja na upandaji wa miti ili kuimarisha afya ya wananchi

Sauti ya mkuu wa mkoa

Viongozi wa mkoa wa Katavi wamewahakikishia wananchi kuwa serikali itaendelea kusikiliza na kutatua changamoto zao, na kuboresha huduma za kijamii