Mpanda FM

RC Katavi “Toeni huduma bora na ufanisi kwa wananchi”

26 November 2025, 10:30 am

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko. Picha na Anna Mhina

“Hakikisheni mnakuwa wabunifu katika kutoa huduma”

Na Restuta Nyondo

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko ameziagiza taasisi zote za umma kutoa huduma bora na ufanisi kwa wananchi na kuhakikisha wanakua wabunifu katika utoaji wa huduma bila visingizio.

Ameyasema hayo katika kikao cha wakuu wa taasisi mkoa wa Katavi ambapo amesema kuwa taasisi za umma ni moyo wa serikali na hivyo ni muhimu kuwajibika katika kutatua changamoto za wananchi.

Sauti ya mkuu wa mkoa

Mpanda radio  FM imezungumza na baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda ambapo wamedai kuwa bado baadhi ya maeneo ya kutolea huduma ikiwemo huduma za afya kuna changamoto ya kupata huduma kwa wakati.

Sauti za wananchi

Hayo yanajiri wakati serikali mkoani  Katavi ikiwa imetoa siku tatu  kuanzia Novemba 25 kwa wananchi kwa ajili ya kusikiliza kero ili kutatua changamoto hizo kutokana kuwepo kwa malalamiko mbalimbali.