Mpanda FM

Madereva bajaji Katavi walia na tozo stend kuu

30 July 2025, 9:29 am

Mkuu wa mkoa wa Katavi akizungumza na madereva bajaji. Picha na Samwel Mbugi

“Kuna mambo bado hayajakaa sawa niwape muda mkayatafakari upya”

Na Samwel Mbugi

Baadhi ya madereva bajaji mkoa wa Katavi wamelalamika kwa mkuu wa mkoa kuhusu kuamriwa kushusha abiria nje ya stendi kuu Mizengo Pinda pamoja na tozo wanazotoa.

Hayo yamejiri  wakati mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko alipofika kusikiliza kero ambazo wanakumbana nazo  abiria pamoja na wananchi wanaofanya shughuli ndani ya stendi

Sauti ya madereva bajaji

Kupitia changamoto hizo mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amemuagiza mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda pamoja na viongozi wa stendi hiyo ndani ya mwezi mmoja wawe wametatua changamoto hiyo ambayo inawakumba madereva bajaji.

Sauti ya mkuu wa mkoa

Hata hivyo Mrindoko ameuagiza uongozi wa manispaa ya Mpanda kuhakikisha usafi unadhibitiwa kikamilifu ndani na nje ya stendi ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.