Mpanda FM

Watumiaji earphone hatarini

19 May 2025, 5:30 pm

Picha na mtandao

Amewaasa wananchi kuachana na matumizi ya earphone ili kuepukana na changamoto za  uchovu wa masikio,maumivu ya kichwa.

NA Rhoda Elias -Katavi

Baadhi ya wananchi  manispaa ya Mpanda mkaoni Katavi wameiomba serikali kutoa elimu zaidi juu ya madhara yanayoweza kutokana na matumizi ya earphone kwa muda mrefu.

Wakizungumza na Mpanda Redio FM wananchi hao wamesema kuwa wanatumia earphone Kwa mazoea pasipo kutambua madhara yanayoweza kujitokeza.

Sauti za wananchi wakizungumza

Gabriel Elias ni mganga mfawidhi wa kituo cha Afya  Town clinic amewaasa wananchi kuachana na matumizi ya earphone ili kuepukana na changamoto za  uchovu wa masikio,maumivu ya kichwa.

Sauti ya daktari

Matumizi ya earphone kwa muda mrefu yanaweza kusababisha matatizo ya kusikia, kuathiri mfumo wa neva,na kuongeza hatari ya kupata kansa kutokana na mionzi ya kifaa kinachotumika.