Mpanda FM

Matukio ya wizi yakomeshwa,ulinzi shirikishi watajwa

19 May 2025, 3:12 pm

picha na mtandao

Ulinzi shirikishi katika mtaa wa Mpadeco kata ya Makanyagio manispaa ya Mpanda mkoani Katavi umetajwa kuwa moja ya njia inayosaidia kutokomeza matukio ya kihalifu

Wakizungumza na Mpanda Redio FM baadhi ya wananchi wa mtaa wa Mpadeco wamesema kuwa ulinzi shirikishi umesaidia kutokomeza matukio ya mwizi katika mtaa huo huku wakiomba serikali kuhakikisha watu wanaofanya shuguli hiyo ya ulinzi kuwapatia vifaa na vitambulisho ambavyo vitawasadia katika majukumu yao.

Sauti ya wananchi wakizungumza

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Mpadeco kata ya Makanyagio Ivo chambala amesema kuwa hadi sasa kuna kesi tatu ambazo zimefikishwa kituo cha polisi kupitia ulinzi shirikishi na kuwaomba wananchi kuwa makini nyakati za mchana kwani yapo baadhi ya matukio ya wizi ambayo yanafanyika nyakati hizo na yatari yameripotiwa.

Sauti Mwenyekiti wa mtaa wa Mpadeco

Aidha chambala amewaomba wananchi kuendelea kuchangia fedha kwa ajili ya ulinzi shirikishi ambapo mtaa huo wa Mpadeco unajumla ya kaya 674.