Mpanda FM

Wananchi Mpanda walilalamikia jeshi la zimamoto na uokoaji

16 March 2025, 3:25 pm

Afisa habari wa jeshi la zimamoto na uokoaji Katavi, Catherine Sambagi. Picha na Anna Mhina

“Wananchi wanachelewa kutoa taarifa kwa jeshi la zimamoto na uokoaji”

Na Anna Mhina

Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameliomba jeshi la zimamoto na uokoaji kuweka mifumo bora ili kuweza kufika kwa wakati pindi wanapopokea taarifa za dharura.

Wakizungumza na Mpanda Radio FM wananchi hao wamelilalamikia jeshi la zimamoto na uokoaji kutofika kwa wakati eneo la tukio na kuiomba serikali iboreshe miundombinu ya vitendea kazi katika jeshi hilo.

Sauti ya wananchi

Akijibu malalamiko hayo afisa habari wa jeshi hilo mkoa wa Katavi Catherine Sambagi amesema kuwa wananchi wanachelewa kutoa  taarifa hali inayowasababisha kushindwa kufika eneo la tukio kwa wakati.

Sauti ya afisa habari

Mojawapo wa njia inayotumiwa kutoa taarifa  ya dharura kwa jeshi la zimamoto na uokoaji inapotokea ni kupiga namba 114.