Mpanda FM

Mvua yaezua paa katika shule ya msingi Ivungwe

11 March 2025, 2:36 pm

Picha ya madarasa yaliyoezuliwa. Picha na Anna Mhina

“Hakikisha  miundombinu ya madarasa inajengwa kwa wakati”

Na Anna Mhina

Shule ya msingi Ivungwe iliyopo kata ya Katumba halmashauri ya Nsimbo wilayani Mpanda mkoani Katavi imeezuliwa paa kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali kunyesha march 8, mwaka huu.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Mwalimu mkuu wa shule hiyo Maiko Cosmas ameeleza namna tukio lilivyotokea na hatua walizozichukua.

Sauti ya mkuu wa shule

Kwa upande wake Injinia  Salimu Kisaka ameeleza kuwa gharama za madarasa  mapya yanayotakiwa kujengwa yakiwa na viwango vinavyotakiwa  yatagharimu zaidi ya million 70.

Sauti ya injinia

Mkuu wa wilaya ya Mpanda amefika shuleni hapo na kujionea uharibifu uliojitokeza ambapo ametoa maelekezo kwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuhakikisha  miundombinu ya madarasa inajengwa kwa wakati ili kusaidia wanafunzi kuendelea na masomo.

Sauti ya mkuu wa wilaya