Mpanda FM

Watu 118 wanashikiliwa na jeshi la polisi katavi

7 February 2025, 1:52 pm

Picha ya kamanda wa polisi mkoa wa Katavi SACP Kaster Ngonyani. Picha na Lilian Vicent

“Wananchi watakiwa kuacha kujihusisha na vitendo vya uhalifu”

Na Lilian Vicent

Jeshi la polisi mkoa wa katavi  limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 118 ambapo kati yao watuhumiwa 37 wamekamatwa wakiwa na mali zinazodhaniwa za wizi.

Hayo yamebainishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Katavi SACP Kaster Ngonyani ambapo watuhumiwa wamejihusisha na  wizi wa  pikipiki, nondo  ambazo ni mali  ya maji safi na usafi wa mazingiara [MUWASA ] ,matumizi ya silaha haramu , madawa ya kulevya ,matumizi ya pombe moshi na makosa mengine.

Sauti ya kamanda

Kwa upande wa kesi za mahakamani  jumla ya watuhumiwa 17 wamepatikana na hatia na kuhukumiwa vifungo  mbalimbali katika kesi zinazowakabili.

Sauti ya kamanda

Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani hapa limefanikiwa kuzuia ajali za barabarani kwa kukamata jumla ya  makosa 2,231 ambayo yanahususisha ukiukwaji wa  sheria za usalama barabarani.

Sauti ya kamanda Ngonyani

Jeshi la polisi mkoa wa Katavi limetoa wito kwa wananchi kuacha kujihusisha na vitendo viovu vya uhalifu pamoja na matukio ya kujichukulia sheria mkononi na kuripoti matukio ya kihalifu.