Mpanda FM

Msongo wa mawazo hupelekea kujitoa uhai

30 January 2025, 12:35 pm

Picha ya mfano wa mtu mwenye msongo wa mawazo.

“Imebainika kuwa chanzo cha watu kujiua ni msongo wa mawazo”

Na Rhoda Elias

Baadhi ya wananchi manispaa ya Mpanda Mkoani katavi wamesema hali duni ya kimaisha na msongo wa mawazo ni miongoni mwa sababu zinasosababisha  kukithiri kwa matukio ya watu  kujitoa uhai.

Wakizungumza na Mpanda radio FM baadhi ya wananchi  wametaja  sababu hizo ambapo wananchi wamekuwa wakishindwa kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo hali inayopelekea kujitoa uhai.

Sauti ya wananchi.

Kwa upande wake mwanasaikolojia Fransisco Wanga ametaja baadhi ya sababu zinazopelekea watu kujitoa uhai huku akiwaasa namna ya kuweza kukabiliana na tatizo hilo.

Sauti ya mwanasaikolojia Fransisco Wanga.

Wanga  ameongeza kuwa endapo mtu alijaribu kufanya jaribio la kujitoa uhai  na ikashindikana, mtu huyo anakuwa katika hatari ya kujitoa uhai kwa mara nyingine tena hivyo anapaswa kuchunguzwa mienendo yake.