Mpanda FM

Tume huru ya uchaguzi yasisitiza ushirikiano Katavi

11 July 2024, 5:10 pm

Jaji wa Mahakama Kuu  Asina Omari ambaye  ni mjumbe wa tume  .picha na Rachel Ezekia

Tayari halmashauri  na majimbo yameshapokea vifaa  kwa ajili ya zoezi la uboreshaji  wa daftari la mpiga kura”.

Na Rahel Ezekia -Katavi

Tume huru ya uchaguzi  imewataka Washiriki wa mafunzo ya maboresho ya daftari la mpiga kura kuzingatia maelekezo  yanayotolewa ili kuleta matokeo bora katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Mwezi wa 11 Mwaka huu. 

Wito huo umetolewa na Jaji wa Mahakama Kuu  Asina Omari ambaye  ni mjumbe wa tume  katika mafunzo  yanayotolewa kwa waratibu uandikishaji  mkoa, maafisa uandikishaji , maafisa undikishaji ngazi ya jimbo, maafisa uchaguzi ,  maafisa ugavi , pamoja na maafisa Tehama wa halmashauri .

Sauti ya jaji wa mahakama kuu Asina Omari ambaye ni mjumbe wa tume

Kwa upande wake Rebeka Msambuse Mratibu  wa Uandikishaji wa uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura Mkoa wa Katavi amebainisha kuwa tayari halmashauri  na majimbo yameshapokea vifaa  kwa ajili ya zoezi la uboreshaji  wa daftari la mpiga kura.

Sauti ya mratibu wa uandikishaji wa uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura mkoani Katavi Rebeka Msambuse