Jamii FM

Wadau waombwa kuchangia sherehe za Maulid mkoani Mtwara

31 August 2024, 12:21 pm

Wanafunzi wa Madrasat Tarbiya wakiwa katika sherehe za Maulidi katika mtaa wa Chihiko Mtwara (Picha na Musa Mtepa)

Miaka yote tumekuwa tukifanya sherehe hizo kwa kutumia nguvu zetu hivyo kutokana na hali ya maisha kubadilika tunaomba wadau wenye uwezo kuchangia sherehe hizo ili kuendelea kumtukuza Mtume Muhammadi S.W.A”.

Na Musa Mtepa

Umoja wa wanawake waislamu kutoka Chihiko kata ya Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani wameomba wadau na jamii ya kiislamu kuchangia sherehe za Maulidi zinazofanyika kila mwaka katika eneo ili kuendeleza kulitukuza jina la Mtume Muhammadi S.A.W.

Wakizungumza  na Jamii fm  Radio August 25,2024 Wanawake hao wamesema ni zaidi ya miaka 35 sherehe hizo zimekuwa zikifanyika  ambapo kwa kipindi cha hivi karibuni wamekuwa wakikutana na changamoto ya kiuchumi hali inayowalazimu kulima vibarua mashambani ili kupata fedha itakayo wasaidia kufanikisha sherehe hizo.

Sauti ya Sofia Shantiri Mwana umoja wa akina mama waislamu Chihiko Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Mzee Seif Akaliwaza Msimamizi wa sherehe hizo amesema ni zaidi ya miaka kumi sasa amekuwa nao  huku akiomba wafadhili kuwasaidia akina mama hao  katika kufanikisha sherehe hizo.

Sauti ya Mzee seif Akaliwaza msimamizi wa sherehe za maulidi kupitia umoja wa akina mama waislamu Chihiko.

Kwa upande wake Ostadhi Hamisi Chikambu amesema kitendo kinachofanywa na akina mama hao ni katika kuunga mkono kile kilichofanywa na Bi Hadija ambae alikuwa mke wa Mtume Muhammadi SAW baada ya kutoa mali zake zote kwa mumewe ili aweze kuutangaza uislamu kwa uzuri.

Sauti ya Ostadhi Hamisi Chikambu