Jamii FM

Mwenge wa uhuru kupitia miradi 62 yenye thamani ya Bilioni 30.09 Mtwara

30 May 2024, 13:32 pm

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa mkuu wa wilaya ya Mtwara Mwanahamisi Munkunda katika viwanja vya shule ya msingi Mpapura wilayani Mtwara (Picha na Musa Mtepa)
 
Katika mkoa wa Mtwara Mwenge utarajia kukimbizwa katika halmashauri tisa,wilaya sita  katika Miradi 62 yenye thamani  zaidi  ya shilingi Bilioni ambapo tarehe 30/5/2024 halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani ndio ya kwanza kukimbizwa kwa mkoa wa Mtwara

Na Musa Mtepa

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala leo tarehe 30/5/2024 amepokea Mwenge wa Uhuru  ukitokea mkoani Lindi katika Viwanja vya shule ya Msingi Mpapura halmashauri ya Mtwara Vijijini.

Akiongea wakati wa mapokezi ya Mwenge huo mkuu wa mkoa Sawala amesema kuwa Mwenge wa uhuru katika mkoa wa Mtwara utakimbizwa katika umbali wa kilomita 906.6  kwa kupitia miradi 62 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bilioni 30.09

Sauti ya 1 mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala

Aidha RC Sawala amesema kuwa mbio za mwenge wa uhuru  utakimbizwa  katika Wilaya sita,Halmashauri tisa na ukitarajiwa kukabidhiwa mkoani Ruvuma baada ya siku tisa kuanzia tarehe 30/5/2024.

Pamoja na hayo  RC Sawala ametumia nafasi hiyo kuelezea  maandalizi na shughuli mbalimbali zilizofanywa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kushirikiana na ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa kuwa ni Pamoja na uhakiki wa maeneo ya utawala na kubaini idadi ya wapiga kura.

Sauti 2 mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala akielezea miradi ya maendeleo itakayopitiwa na mbio za mwenge wa uhuru katika mkoa wa Mtwara. (Picha na Musa Mtepa)

Mh Kanali Patrick Sawala amekabidhi Mwenge wa uhuru kwa mkuu wa wilaya ya Mtwara ambayo ambayo ndio wilaya ya kwanza kukimbiza Mwenge huo katika mkoa wa Mtwara ambapo utakimbizwa  katika halmashauri ya Mtwara mjini, Mtwara vijijini na halmashauri ya mji Nanyamba

Baadhi ya viongozi wa halmashauri ya manispaa ya Mtwara Mikindani waliojitokeza katika mapokezi ya mwenge wa uhuru katika viwanja vya shule ya Msingi Mpapura. (Picha na Musa Mtepa)

Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 unachagizwa na kauli mbiu ya “Tunza Mazingira na shiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa ujenzi wa taifa endelevu”

Wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Mtwara (Mtwara Girls) wakifuatilia makabidhiano ya Mwenge wa uhuru katika viwanja vya shule ya Msingi Mpapura. (Picha na Musa Mtepa)