Jamii FM

Zaidi ya wakimbiaji 100 washiriki Mikindani Marathon

29 June 2024, 13:13 pm

Mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala akiongoza mbio za kilomita 2.5 Mikindani Marathon(Picha na Musa Mtepa)

Mikindani Marathoni Marathoni ni sherehe zinazoambatana na maadhimisho ya siku ya mikindani(Mikindani day) ambayo dhima ni kutangaza utalii wa mji mikindani ,utamaduni wa makabila ya mikindani(Mtwara) pamoja na historia mbalimbali za mji huo.

Na Musa Mtepa

Katika kusheherekea kilele cha siku ya Mikindani (Mikindani day) Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala mapema leo Juni 29,2024 ameshiriki Mikindani Marathoni katika mji Mkongwe wa Mikindani ambapo zaidi ya wakimbiaji 100 wameshiriki  katika marathoni hiyo.

Akizungumza wakati wa mbio hizo RC  Sawala amesema ni siku ya kihistoria kwa mkoa wa Mtwara katika kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mji Mkongwe wa Mikindani na mkoa wa Mtwara kwa ujumla kupitia marathoni na michezo mbalimbali iliyofanyika katika kilele hicho.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala

Kwa upande wake katibu mkuu wa kamati ya Olympiki Tanzania Filbert Bayi amefarijika kuona uwepo wa Mikindani Marathon huku akitaka hamasa kuongezeka kupitia kwa wadau na  wanamtwara kushiriki katika mbio hizo kwani zinaweza kuzalisha wakimbiaji wazuri wanaoweza kuwakilisha Mtwara na nchi kimataifa.

Sauti ya Filbert Bayi katibu mkuu wa kamati ya Olimpiki Tanzania

Naye Mshindi wa Mbio  za kilomita 21 Haji Kajao (CHAMPIONI) amesema anatamani kuona Mikindani Marathoni yakiendelea kwa kila Mwaka kwani imekuwa ikileta hamasa kwa vijana na inaweza kuwa sehemu ya kuonesha vipaji vyao.

Sauti ya Haji Alli Kajao mshindi wa kilomita 21 katika Mikindani Marathon

Guakisa Mwasyeba na Shabani Majidi washindi wa pili na watatu kwa mbio za kilomita 21 ambapo  wameshukuru kushiriki katika Marathoni hiyo huku wakitoa ushauri kwa washiriki kutambua afya zao kabla ya kushiriki.

Sauti ya Guakisa Mwasyeba na Shabani Majidi Washindi wa pili na wa tatu katika Mikindani Marathon kwa umbali wa kilomita 21

Mikindani Marathoni zimehusisha katika umbali wa kilomita 21,km 10,km 5 na km 2.5 zenye lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika mji mkongwe wa Mikindani Pamoja na utamaduni wa watu wa pwani na mkoa wa Mtwara kwa ujumla.

Haji Alli Kajao mshindi wa kwanza wa kilomita 21 katika Mikindani Marathon 2024