Jamii FM
Jamii FM
27 November 2025, 18:01 pm

Akiwa ni mtu mwenye ulemavu wa viungo, amejitolea kuitumia taaluma yake kuibua na kusimulia hadithi za jamii, hususan za watu wasiojiweza na watu wenye ulemavu.
Na Msafiri Kipila
Katika jamii inayozingatia usawa wa haki na fursa, ni muhimu kila mwananchi kupata huduma za kijamii kwa usawa bila vikwazo, Uwepo wa mazingira rafiki husaidia watu wote, hususan watu wenye ulemavu, kupata huduma kwa urahisi na kwa kujitegemea bila kulazimika kuomba msaada wa mara kwa mara.
Katika kipindi hiki, tupo na Tuma Dandi, mwandishi wa habari na mtangazaji maarufu wa televisheni na vyombo vya habari nchini Tanzania. Tuma Dandi ni mtangazaji wa kipindi cha Wape Nafasi kinachorushwa na TBC1 (Shirika la Utangazaji Tanzania). Akiwa ni mtu mwenye ulemavu wa viungo, amejitolea kuitumia taaluma yake kuibua na kusimulia hadithi za jamii, hususan za watu wasiojiweza na watu wenye ulemavu, kwa lengo la kuhamasisha jamii, wadau na mamlaka husika kutoa msaada na kufungua fursa mbalimbali.
Ungana nasi kusikiliza kipindi hiki kwa kubonyeza hapa muhimu ili kujifunza, kuelewa na kuchangia katika ujenzi wa jamii jumuishi yenye mazingira rafiki kwa wote.