

27 February 2021, 11:23 am
Timu ya shirika la umeme Tanzania(TANESCO) Mkoa wa Mtwara, wamechapwa goli 3-1 na timu ya Veteran Mtwara.
Mechi hiyo ya mpira wa miguu iliyochezwa leo februari 27, 2021 kwenye viwanja vya bonanza mkoani hapa, TANESCO wamefungwa goli zote tatu katika kipindi cha kwanza cha mchezo.
Kipindi cha pili timu zote zilianza kwa kushambuliana na dakika ya 79 ya mchezo timu ya Tanesco wakapata goli la kufutia machozi kwa mkwaju wa adhabu ndogo iliyopigwa nje ya 18 na kufanya matokeo mpaka mwisho ni 3 kwa 1.
Credit: Gregory Millanzi
Matukio katika picha