Jamii FM

THBUB yatoa mafunzo kwa wanahabari Mtwara

26 September 2025, 11:03 am

Waandishi wa habari mkoani Mtwara wakiwa katika mafunzo yaliyoandaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na utawala bora(Picha na Musa Mtepa)

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Mtwara, ikiwataka kuzingatia maadili ya taaluma, haki za binadamu na misingi ya utawala bora, hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025. Waandishi wameahidi kutumia mafunzo hayo kuboresha uwajibikaji katika kazi zao

Na Musa Mtepa

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imewataka waandishi wa habari mkoani Mtwara kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kwa kuzingatia maadili ya taaluma na kuheshimu misingi ya haki za binadamu.

Akizungumza wakati wa mafunzo maalum kwa waandishi wa habari yaliyofanyika September 25, 2025 mjini Mtwara, Afisa Uchunguzi Mkuu kutoka Tume hiyo, Bi. Juliana Laurent, amesema waandishi wa habari ni kiungo muhimu katika mnyororo wa ukusanyaji na upashanaji wa taarifa kwa umma.

Sauti: 1 Juliana Laurent – Afisa Uchunguzi Mkuu, THBUB
Bi. Juliana Laurent Afisa Uchunguzi Mkuu kutoka Tume ya haki za binadamu na utawala bora akitoa mafunzo kwa Waandishi wa Habari (Picha Musa Mtepa)

Aidha, Bi. Juliana amebainisha kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwakumbusha waandishi habari umuhimu wa kuzingatia haki za binadamu na misingi ya utawala bora katika kazi zao za kila siku, hasa wakati huu taifa linapoelekea katika kipindi muhimu cha uchaguzi.

Sauti: 2 Juliana Laurent – Afisa Uchunguzi Mkuu, THBUB

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mtwara, Bw. Bryson Mshana, amesema mafunzo hayo yamekuwa chachu kwa waandishi wa habari kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuimarisha mahusiano kati yao na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Sauti: Bryson Mshana – Katibu, Chama cha Waandishi wa Habari Mtwara
Katibu wa chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Mtwara (MTPC) Brayson Mshana akitoa neno la Shukrani kwa THBUB(Picha na Musa Mtepa)

Baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki mafunzo hayo wameeleza kufurahishwa na elimu waliyopata na kuahidi kuzingatia mafunzo hayo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Sauti: Waandishi wa Habari walioshiriki Mafunzo
Baadhi ya Waandishi wa habari mkoani Mtwara wakiwa katika mafunzo ya umuhimu na wajibu wa waandishi wa habari kuelekea katika uchaguzi mkuu oktoba 29,2025(Picha na Musa Mtepa)