Jamii FM
Jamii FM
23 December 2025, 16:58 pm

Ulemavu si jambo la hiari, na kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mlemavu wakati wowote katika maisha yake.
Na Msafiri Kipila
Watu wenye ulemavu ni sehemu muhimu ya jamii na wana mchango mkubwa katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Licha ya uwezo na vipaji walivyonavyo, kundi hili limekuwa likikumbana na changamoto mbalimbali, nyingi zikiwa ni za kuepukika. Changamoto hizo ni pamoja na miundombinu isiyo rafiki, ukosefu wa mazingira jumuishi, pamoja na kukosekana kwa usawa wa fursa katika nyanja mbalimbali za maisha.
Kwa kutambua hali hiyo, wanachuo wa Chuo cha Utumishi wa Umma wametoa maoni yao kuhusu umuhimu wa kuboresha mazingira yanayowazunguka watu wenye ulemavu. Wanachuo hao wamejadili pia namna bora za kutatua changamoto wanazokumbana nazo watu wenye ulemavu, wakisisitiza kuwa ulemavu si jambo la hiari, na kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mlemavu wakati wowote katika maisha yake.