Jamii FM

NSSF Mtwara yatoa msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango ya wanachama

22 June 2024, 09:59 am

Meneja wa mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii(NSSF) mkoa wa Mtwara Bw Rebule Maira akizungumza na Waandishi wa habari jana ofisini kwake (Picha na Musa Mtepa)

Katika utekelezaji wa shughuli za NSSF mfuko umekuwa ukikutana na changamoto mbalimbali na moja yake ni Pamoja na Mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati na hili limekuwa tatizo kubwa kiasi kwamba inasababisha malalamiko kwa wananchi na wanachama na kudhani kwamba serikali haifanyi kazi yake ipasavyo na hii ni kwasababu wanapo kuja kwenye mfuko hawakauti fedha yao imewekwa.

Na Musa Mtepa

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) imeamua kutoa msamaha wa tozo zinazotokana na ucheleweshaji wa kulipa michango ya wanachama ikiwa katika  kumpunguzia mzigo mwajiri wa kulipa michango hiyo pamoja na kujenga mahusiano mazuri yaliyopo kati ya mfuko na Mwajiri.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake Juni 21,2024 Meneja wa  NSSF mkoa wa Mtwara Rebule Maira amesema katika kutoa msamaha huo wametoa masharti kwenye vipengere vitatu ambavyo moja wapo ni kwa waajiri ambao watalipa malimbikizo ya michango kabla ya tarehe 31 julai 2024 watasamehewa tozo ya adhabu kwa 100%.

Sauti ya Rebule Maira meneja wa NSSF mkoa wa Mtwara

Aidha Bw Rebule amesema kuwa kuna waajiri ambao wanamalimbikizo yanayofikia Shilingi Bilioni 3 na wengine waliofikishwa mahakamani  ambao  waliomba kulipa kwanza malimbikizo ya  michango ya wanachama na tozo za adhabu kutoingizwa kwenye kesi zilizopo Mahakamani na  kuahidi kuzilipa hapo baadae nao watasemehewa kwa 100% .

Sauti ya Rebule Maira meneja wa NSSF mkoa wa Mtwara

Pamoja na hayo meneja Rebule Maira ametoa wito kwa waajiri wa Mtwara kutumia fursa hiyo kulipa malimbikizo ya michango ili kuondookana na mzigo mkubwa wa tozo za adhabu ambazo zimewekwa kisheria  na zinamtaka Mwajiri kulipa ila uongozi wa mfuko umeamua kuwasamehe.

Sauti ya 3 Rebule Maira meneja wa NSSFmkoa wa Mtwara