Jamii FM

Wanawake viongozi wafunguka kuhusu nafasi zao katika siasa

20 May 2025, 16:30 pm

Waandishi wa Jamii FM wakiwa katika kipindi cha Dira ya asubuhi. Picha na Mwanaidi Kopakopa

Na Mwanaidi Kopakopa, Mwanahamisi Chikambu

Wanawake walioko katika nafasi za uongozi wamesema kuwa nafasi wanazopewa kama madiwani au wabunge zinawajengea uwezo na kujiamini kugombea nafasi nyingine za juu za uongozi wa kisiasa.

Katika makala haya, wanawake hao wameeleza kwa kina jinsi wanavyopambana kuwania nafasi za uongozi kwa njia ya ushindani wa moja kwa moja, na kuachana na uteuzi kupitia viti maalum. Wamesema kuwa mara baada ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi, woga huondoka na kuwasaidia kujikita kikamilifu katika kampeni na harakati za kisiasa.

Makala: Jinsi viti maalumu vinavyoweza kuwa kipimo sahihi kuwa kiongozi

Bonyeza hapa kusikiliza makala inayoangazia viti maalumu vinavyoweza kuwa kipimo sahihi cha wanawake kuongoza katika uongozi wa kuchaguliwa na wananchi.