Jamii FM

Wanafunzi wa watatu wa shule ya sekondari Madimba wajeruhiwa na radi

17 March 2025, 22:15 pm

Picha ya Mfano wa mwonekano wa radi(kwa msaada wa mtandao)

Tukio la kujeruhiwa na radi Wanafunzi watatu wa shule ya sekondari Madimba limetokea siku ya Jumanne ya March 11 wakiwa Darasani

Na Musa Mtepa

Wanafunzi watatu wa Shule ya Sekondari Madimba, iliyopo katika Halmashauri ya Mtwara Vijijini, Mkoani Mtwara, wamenusurika kifo baada ya kujeruhiwa na radi iliyotua katika viwanja vya shule hiyo.

Tukio hili lilitokea siku ya Jumanne, Machi 11, 2025, wakati wanafunzi hao walipokuwa  darasani.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Madimba, Bw. Hamdi Hassani Mdumba, ameeleza kwamba radi imejeruhi wanafunzi watatu wa Kidato cha Nne. Wanafunzi hawa walipelekwa katika Zahanati ya Madimba kwa  matibabu zaidi .

Sauti ya 1 Hamdi Hassani Mdumba mwenyekiti wa Kijiji cha Madimba

Katika hatua nyingine, Bw. Hamdi ametoa wito kwa serikali  kuangalia njia bora ya kuweka vizuizi au vikinga radi kwenye vyumba vya madarasa, ili kuwalinda wanafunzi dhidi ya madhara ya radi wanapokuwa shuleni hasa wakati wa mvua.

Sauti ya 2 Hamdi Hassani Mdumba mwenyekiti wa Kijiji cha Madimba

Kwa upande mwingine, Issa Msaka, mzazi wa mmoja wa wanafunzi waliojeruhiwa na radi,amesema kuwa alipata taarifa mtoto wake kujeruhiwa na radi akiwa narejea kutoka shambani ndipo alichukua jitihada za haraka kumpeleka  Zahanati kwa ajili ya matibabu.

Sauti ya Issa Msaka mzazi wa mtoto aliyejeruhiwa na radi.
Issa Msaka mzazi wa mmoja ya wanafunzi waliojeruhiwa na radi wa shule ya sekondari Madimba(Picha na Musa Mtepa)

Wakazi wa Kijiji cha Madimba wameeleza kuwa tukio hili ni la kwanza kutokea katika kijiji chao tangu kuanzishwa kwake, hali iliyowapa mshangao na wasiwasi mkubwa.