Jamii FM

Watuhumiwa 14 wakamatwa kuhusika na mali za wizi Mtwara

15 May 2024, 21:33 pm

Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa jeshi la polisi mkoa wa Mtwara Issa Suleiman akitoa taarifa kwa waandishi juu ya doria iliyofanyika katika kipindi cha mwezi 3 na 4 ,2024 katika mkoa wa Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Napenda kuwajulisha wananchi kuwa mkoa wa Mtwara upo shwari dhidi ya uhalifu na Elimu ya kuzuia na kutanzua imeendelea kutolewa kwa wananchi kupitia wakaguzi wa kata katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Na Musa Mtepa

Jeshi la polisi mkoa wa Mtwara limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 14 kwa kipindi cha Mwezi wa 3/ 4,2024 kwa kuhusika na upatikanaji wa mali za wizi na mtuhumiwa mmoja kukamatwa na Migomba 76 ya Bhangi.

Akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari leo tarehe 15/5/2024 Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara Kamishina Msaidiz Mwandamizi wa Jeshi la Polisi(SACP)  Issa  Suleiman amezitaja mali hizo zilizokamatwa kupitia doria iliyofanyika katika kipindi cha Mwezi wa 3/ 4 ,2024 kuwa ni pamoja na Jokofu moja aina ya mr Uk ,pikipiki nne,Tv 13 zenye aina na ukubwa tofauti .

Sauti ya 1 SACP Issa Suleiman Kmanda wa Polisi mkoa wa Mtwara

Aidha Kamanda Issa Suleiman amesema zimekatwa pia redio Subwoofer 13 aina mbalimbali na spika zake ikiwemo Kompyuta mpakato (Laptop) aina ya HP  Pamoja na ving’amuzi 32 vya kampuni ya Azam na startimes

Sauti ya 2 SACP Issa Suleiman Kmanda wa Polisi mkoa wa Mtwara
Vifaa na mali za wizi zilizokamatwa na jeshi la polisi mkoa wa Mtwara vilivyokamatwa kupitia doria iliyofanyika katika kipindi cha mwezi 3/3 ,2024(Picha na Musa Mtepa)

Hata hivyo Jeshi la Polisi mkoa wa Mtwara limewaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano katika kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu ili kukomesha matukio ya hayo.

SACP Issa Suleiman akionesha pikpiki aina ya TVS zilizokamatwa kupitia doria iliyofanywa na jeshi la polisi mkoa wa Mtwara kwa kipindi cha mwezi 3/ 4 ,2024 (Picha na Musa Mtepa)