Jamii FM

RC Sawala awataka wananchi kutoa ushirikiano dhidi ya vitendo vya ukatili

15 May 2024, 20:00 pm

Kanali Patrick Sawala Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akizungumza na Wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya familia Duniani katika viwanja vya shule ya sekondari Ziwani Mtwara Vijijini(Picha na Mtwara rs habari)

Taasisi zinazohusika na utoaji wa haki na kusimamia masuala haya kuyatendea haki ili kuendelea kumlinda mtoto na mwanamke na mtanzania kwa ujumla ili awe salama zaidi.

Na Musa Mtepa

Wananchi wameombwa kushirikiana na serikali katika kuelimisha jamii kuachana na vitendo vya ukatili, kutoa taarifa na ushirikiano wakati vitendo hivyo vinapo fanyika.

Wito huo umetolewa leo tarehe 15/5/2024 na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala kwenye  maadhimisho ya siku ya familia Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya sekondari Ziwani  Wilayani Mtwara ambapo amesema kila mmoja anawajibu wa kutimiza wajibu wake katika malezi ikiwa na Pamoja na kutoa huduma muhimu kwa Watoto.

Sauti ya1  Kanali Patrick Sawala Mkuu wa Mkoa wa Mtwara

Aidha mkuu wa mkoa  Kanali Sawala amewaomba  Waandishi wa Habari kupitia vyombo vya kuendelea kuelimisha  jamii  kuhusu umuhimu wa malezi bora ya Watoto kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya taifa na familia kwa ujumla.

Sauti ya 2  Kanali Patrick Sawala Mkuu wa Mkoa wa Mtwara

Pia  mkuu wa Mkoa ametumia maadhimisho hayo kuwataka  wananchi kujitokeza kwa uwingi katika mapokezi ya Mwenge wa uhuru unaotarajiwa kupokelewa tarehe 30/5/2024 katika Kijiji cha Mapapura kilichopo halmashauri ya Mtwara vijijini ukitokea mkoani Lindi  Pamoja na kuwataka wananchi wenye sifa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Mwaka huu nchini.

Sauti ya 3  Kanali Patrick Sawala Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Bi Theresia Ngonyani afisa ustawi wa jamii mkoa wa Mtwara akitoa taarifa juu ya vitendo vya ukatili vinavyofanyika katika jamii ya mtwara(Picha na Mtwara rs habari)

Kwa upande wake afisa ustawi wa jamii mkoa wa Mtwara Bi Theresia Ngonyani amesema Pamoja na umuhimu wa familia jamii imekuwa ikikutana na changamoto nyingi  ikiwepo uwepo wa talaka holela ambapo 80%  ya Watoto waliohudumiwa  katika Halmashauri  kwa kipindi cha mwezi 1 hadi Mwezi wa 3 ,2024  wanaishi kwa bibi au jamaa  wengine hali inayoonesha uwepo changamoto hiyo.

Sauti ya 1 Theresia Ngonyani afisa ustawi wa jamii mkoa wa Mtwara

Sambamba na hilo Bi Theresia amewaeleza  wazazi kuwa  umri  wa mwaka 0 hadi 8  mtoto ubongo wake unakuwa kwa 90%  hivyo kama mzazi anatakiwa kuwekeza katika umri huo ili Watoto waweze kujipambanua , kujitafakari na kujieleza vizuri ikiwa njia ya  kupunguza vitendo vya Watoto  kufanyiwa ukatili bila kushirikisha wazazi wao.

Sauti ya 2 Theresia Ngonyani afisa ustawi wa jamii mkoa wa Mtwara
Selemani Nampanye Mwenyekiti wa halmashauri ya Mtwara Vijijini akizungumza na wananchi waliohudhuria maadhimisho ya siku ya familia Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Ziwani wilayani Mtwara(Picha na Mtwara rs habari)