Jamii FM

PPRA yatoa mafunzo kwa makundi maalumu Mtwara

13 November 2025, 11:21 am

Makundi maalumu washiriki wa mafunzo yaliyotolewa na PPRA November 12,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Benjamini Mkapa kilichokuwa chuo cha ualimu Mtwara wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

PPRA imeendesha mafunzo kwa makundi maalumu mkoani Mtwara kuhusu taratibu za ununuzi wa umma, yakilenga kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali. Mafunzo hayo yamezinduliwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Bahati Geuzye, na yataendelea hadi Desemba katika halmashauri zote za mkoa

Na Musa Mtepa

Mtwara, Novemba 12, 2025Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imeendesha mafunzo maalumu kuhusu taratibu za manunuzi ya umma kwa makundi maalumu yakiwemo watu wenye ulemavu, kwa lengo la kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali.

Akifungua mafunzo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Bahati Geuzye, amesema mafunzo hayo ni fursa muhimu na ya kipekee kwa wadau kutoka makundi maalumu kujifunza kuhusu sheria, kanuni na taratibu za ununuzi wa umma.

Sauti ya 1 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara
Katibu tawala mkoa wa Mtwara Bi Bahati Geuzye akikibidhi hati ya TRA kwa wajasiliamali wakati wa mafunzo ya PPRA (Picha Musa Mtepa)

Aidha, Bi. Geuzye amesema zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya serikali hutumika kwenye ununuzi wa umma, hivyo ni muhimu kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki na kunufaika na miradi ya maendeleo kupitia mfumo rasmi wa serikali.

Sauti ya 2 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara

Kwa upande wake, Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven, amesema mafunzo hayo yalianza Novemba 10, 2025, na yataendelea hadi mwezi Desemba katika halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 – Magnus Steven, Afisa PPRA
Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

Bw. Steven ameongeza kuwa lengo ni kujenga uelewa na kuimarisha uaminifu kati ya makundi maalumu na serikali, ili waweze kushiriki kikamilifu na kunufaika na zabuni mbalimbali.

Sauti ya 2 – Magnus Steven, Afisa PPRA

Washiriki wa mafunzo hayo wamesema wamepata uelewa mkubwa kuhusu namna zabuni za serikali zinavyotangazwa na nafasi ya watu wenye ulemavu katika mchakato huo, huku wakiahidi kuwa mabalozi wa kutoa elimu zaidi kwa jamii.

Sauti ya washiriki wa mafunzo