Jamii FM

Wadau wanashiriki vipi kutatua changamoto za watu wenye ulemavu

5 November 2025, 19:08 pm

Wadau wenye ulemavu wakiwa katika mafunzo. Picha na Mwnahamisi Chikambu

Tutahakikisha elimu jumuishi inatekelezwa kwa vitendo ili kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye ulemavu na kuboresha kiwango cha elimu mkoani Mtwara

Na Msafiri Kipila

Shirika lisilo la kiserikali Sport Development Aid (SDA) kwa kushirikiana na Jamii FM, linaendelea kuhimiza jamii kuwashirikisha na kuwatambua watu wenye ulemavu katika juhudi za kutatua changamoto zinazowakabili.

Kupitia programu zake, SDA imetoa mafunzo maalum kwa baadhi ya watendaji na walimu wanaofundisha wanafunzi wenye ulemavu, ili wawe mabalozi wa kutoa elimu na kuibua uelewa katika jamii. Lengo ni kuwasaidia wale wanaowaficha watu wenye ulemavu majumbani, jambo linalowanyima haki zao za msingi kama vile elimu.

Kasimu Samuel Shabani, mwalimu wa Shule ya Sekondari Chekeleni iliyoko Mtwara Vijijini, amesema kuwa yeye kama mwalimu atahakikisha elimu jumuishi inatekelezwa kwa vitendo ili kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye ulemavu na kuboresha kiwango cha elimu mkoani Mtwara.

Kwa upande wake, Jackline Mpunjo, Meneja Mradi wa SDA, amesema wameamua kuendesha mpango huo baada ya kubaini kuwa jamii nyingi bado hazijawatambua ipasavyo watu wenye ulemavu. Amesema ni muhimu kuwashirikisha kikamilifu ili waweze kutimiza malengo yao ya kila siku na kujenga jamii yenye usawa na fursa sawa kwa wote.

Bonyeza hapa kusikiliza Makala haya