Jamii FM

SDA yaadhimisha IDPWD kwa usafi wa mazingira

4 December 2025, 17:41 pm

Shirika la SDA wakiwa pamoja na watu wenye ulemavu katika zoezi la usafi wa mazingira. Picha na Msafiri kipila

Ikiwa leo ni Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, siku hii imeambatana na mabadiliko ya tabianchi na uwepo wa mabadiliko hayo kuna athari kwa watu wenye ulemavu.

Na Grace Hamisi

Shirika lisilo la kiserikali Sports Development Aids (SDA) kupitia mradi wake wa mazingira leo tarehe  03/12/2025, wameadhimisha siku ya watu wenye ulemavu duniani kwa kushirikiana na watu wenye ulemavu kufanya usafi eneo la fukwe ya bahari na kutoa elimu namna ya kutunza takataka mkoani Mtwara.

Akizungumza mkurugenzi wa shirika hilo Tea Swai, ameelezea namna walivyoshirikiana na watu wenye ulemavu kufanya usafi huo na kutoa elimu jinsi ya kutunza mazingira pamoja namna ya  kupunguza ukatili kwa watu wenye ulemavu.

Sauti ya Tea Swai – Mkurugenzi wa SDA

Nae Afisa afya Mazingira Salome Mayala, amepongeza kwa kile ambacho kimefanyika kwani kinahamasisha watu kuweza kutunza mazingira na kujikinga na madhara yanayopatikana kwa kuchafua mazingira.

Sauti ya Afisa afya Mazingira Salome Mayala

Kwa upande wake mtaalamu wa masuala ya walemavu na saikolojia, mwalimu Chris Mkwela amesema ikiwa leo ni siku ya watu wenye ulemavu imeambatana na mabadiriko ya tabia ya nchi na uwepo wa mabadiliko hayo kuna athari kwa watu wenye ulemavu kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la umoja wa mataifa ambalo linahusika kupunguza hatari na majanga.

Sauti ya mwalimu Chris Mkwela – mtaalamu wa masuala ya walemavu na saikolojia

Hata hivyo Amani Danfod Kazumari ambae ni mtu mwenye ulemavu ameshukuru shirika la SDA kwa kuwakutanisha pamoja na kufanya usafiri eneo la fukwe ya bahari ambapo alikuwa mazingira sio mazuri.

Sauti ya Amani Danfod Kazumari

Fatuma Mpondomoka mkazi wa likombe ameomba taasisi nyingine pia kuwaweka karibu watu wenye ulemavu katika shughuli mbalimbali ikiwemo siku hizi muhimu na kuwapa taarifa mapema ili wa wao waweze kujiandaa na kuonyesha vile ambavyo wanavifanya kwani wanaweza.

Sauti ya Fatuma Mpondomoka