

19 April 2021, 12:01 pm
Na karim Faida
Michael Hashim ni mtoto wa miaka 16 mkazi wa mtaa wa sokoni kata ya Mtawanya manispaa ya Mtwara mikindani mkoani hapa ambae hakubahatika kwenda shule anasema anatumia fursa ya uwepo wa mto Liyakaya uliopo Jirani na mtaa wake kuvua samaki na kuwauza.
Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mto huo umefurika na maji mengi yanaelekea baharini kupitia Kwenye njia maalumu ambayo Michael na wenzake wanaenda kuwatega samaki hao.
Michael amekuwa akiwasaidia wazazi wake kwa kuwa akipata samaki hao baadhi anawauza ili kupata pesa ya kununua unga na wengine huwabakisha kama kitoweo.