Jamii FM

Makala: mabinti wa Mtwara wavunja ukimya

10 November 2025, 16:24 pm

Bi Thea Swai akizungumza katika moja ya vikao vya wadau. Picha na Mwanahamisi Chikambu

“Wasichana wanajifunza kwamba sauti yao ina thamani, na kwamba wao pia wana nafasi muhimu katika jamii hasa mabinti wa Mtwara”

Na Mwanahamisi Chikambu

Katika dunia ya sasa inayokua kwa kasi kutokana na maendeleo ya teknolojia, bado mtoto wa kike wa Kiafrika anakabiliwa na vikwazo vingi vinavyomnyima nafasi ya kuonekana, kusikika, na kushiriki kikamilifu katika maamuzi yanayohusu maisha yake.

Lakini mkoani Mtwara, hali inaanza kubadilika, Sauti za wasichana zinapata nguvu mpya kupitia mradi wa Binti Paza Sauti (Girls Speak Out) mpango unaolenga kuwajengea uwezo mabinti kujieleza, kushiriki katika maamuzi, na kuvunja ukimya kuhusu changamoto zinazowakabili kila siku kupitia michezo

Kupitia mradi huu, wasichana wanajifunza kwamba sauti yao ina thamani, na kwamba wao pia wananafasi muhimu katika jamii, Karibu katika makala haya, tujifunze kwa pamoja namna ambavyo mabinti wa Mtwara.

Bonyeza hapa kusikiliza