Jamii FM
Jamii FM
5 February 2026, 16:58 pm

Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yameleta mafanikio makubwa kwa Watanzania katika sekta ya madini, ambapo katika migodi mikubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni Watanzania na zaidi ya asilimia tisini ya uongozi na utawala pia unashikiliwa na Watanzania.
Na Gregory Millanzi
Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yamewezesha watanzania wengi kufanya kazi katika sekta ya madini, ambapo katika migodi migubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni watazania huku asilimia zaidi ya tisini ya uongozi na utawala katika migodi hiyo ni watanzania.
Kabla ya mabadiliko ya sheria ya madini mwaka 2017, idadi ya watanzania waliokuwa wanafanya kazi katika migodi mikubwa ya madini, shughuli za utafutaji na uchakataji wa gesi asilia ilikuwa ni ndogo.
Lakini baada ya kufanyika kwa mabadiliko watanzania wengi wanafanya kazi na kusimamia migodi hiyo.
Kamishina wa madini nchini Terence Ngole akiwa mkoani Mtwara katika warsha ya kuelimisha umma kuhusu shughuli za uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini, mafuta na gesi asilia iliyoandaliwa na Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) anafafanua zaidi.
Sheria hiyo inawataka wawekeza kutumia huduma zinazopatikana nchini, na zisizopatikana nchini zihusishe makampuni ya ndani ya nchi, hatua hii imesaidia kuongezeka kwa manunuzi yanayofanywa na watazania.
Wazawa wanaofanya kazi katika sekta hiyo wanaonesha ufanisi mkubwa na halmashauri zikinufaika zaidi na matokeo ya sheria hiyo.