Mpanda FM

Wafugaji, wakulima watakiwa kutunza mazingira

10 April 2025, 3:16 pm

Wakufunzi na washiriki wa mafunzo hayo. Picha na Restuta Nyondo

“Maeneo mengi ya vyanzo vya maji katika bonde hilo bado yanakabiliwa na kitisho cha uharibu wa mazingira “

Na Restuta Nyondo -Katavi

Matumizi ya mawasiliano jumuishi kwa jamii imetajwa kuwa mbinu muhimu zaidi ya kutumia usimamizi wa sheria pekee katika kukabiliana na changamoto za uhifadhi na utunzaji wa vyanzo vya maji.

Haya yanajiri katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la uhifadhi mazingira dunaini IUCN kwa ushirikiano wa GIZ na bonde la maji la ziwa Rukwa katika utekelezaji wa mradi IKI-KATUMA  unaolenga kidakio cha  Mto Katuma mkoani Katavi.

Doyi Mazenzele  ni meneja  mradi kutoka katika shirika la uhifadhi mazingira Duniani IUCN amesema kuwa jamii ya wakulima, wafugaji na watumia maji kwa ujumla  wanapaswa kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali za maji.

Sauti ya Doyi Mazenzele  meneja  mradi kutoka katika shirika la uhifadhi mazingira Duniani IUCN

Afisa uhusiano kutoka bonde la maji la ziwa Rukwa Thadeus Ndese amesema kuwa  maeneo mengi ya vyanzo vya maji katika bonde hilo bado yanakabiliwa na kitisho cha uharibu wa mazingira kutokana na shughuli za kibinadamu.

Afisa uhusiano kutoka bonde la maji la ziwa Rukwa Thadeus Ndese

Nasra Nasoro ni Mtaalamu wa maji juu ya ardhi kutoka bonde la maji la ziwa Rukwa amesema mafunzo waliyopata yatasaidia katika kuyafikia makundi mbalimbali kwa urahisi zaidi ili waweze kushiriki moja kwa moja kutunza na kuhifadhi vyanzo vya maji.

Nasra Nasoro ni Mtaalamu wa maji juu ya ardhi kutoka bonde la maji la ziwa Rukwa

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika halmashauri ya manspaa ya Mpanda kwa siku mbili yaliwahusisaha watalaamu kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa Katavi, halmashari, ,vyombo vya habari na wadau kutoka mashirika mbalimbali.