Joy FM

Namna ongezeko la watu linavyoathri  uchumi wa kaya

24 September 2024, 12:27

Mkuu wa mkoa kigoma Thobias Andengenye akizungumza katika mkutano wa wadau juu ya masuala ya Sensa, Picha na Tovuti ya Mkoa wa Kigoma

Serikali imesema halmashauri nchini hazina budi kutumia matokeo ya sensa ya mwaka 2022 kwa ajili ya kupanga maendeleo ya watu, familia na taifa kwa ujumla.

Na Michael Mpunije – Kasulu

Inaelezwa kuwepo kwa idadi kubwa ya watu kwenye kaya hupelekea athari za Kushuka kiuchumi na kusababisha mkuu wa kaya hiyo kushindwa kutoa huduma muhimu kwenye  familia.

Hayo yameelezwa Afisa takwimu mwandamizi kutoka ofisi ya  taifa ya Takwimu makao.makuu dodoma Bw. Omary Mdoka  wakati akizungumza katika mafunzo ya matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 katika halmashauri ya mji wa kasulu

Bw.Omary ameeleza namna ongezeko la watu kwenye kaya linavyoathri  kiuchumi.

Sauti ya Afisa takwimu mwandamizi kutoka ofisi ya  taifa ya Takwimu makao.makuu dodoma Bw. Omary Mdoka 

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina jenerali mstaafu wa jeshi la.zimamoto na uokoaji Thobias andengenye amesema wanaume wanatakiwa kushirikiana  na wake zao katika kuongeza kipato cha familia.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina jenerali mstaafu wa jeshi la.zimamoto na uokoaji Thobias andengenye
Mkuu wa mkoa kigoma Thobias Andengenye akiwa katika mkutano wa wadau juu ya masuala ya Sensa, Picha na Tovuti ya Mkoa wa Kigoma

Aidha Andengenye amezitaka halmshauri zote za Mkoa wa Kigoma kuhakikisha wanaweka mipango ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kuzingatia Takwimu za sensa ya watu na makazi.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina jenerali mstaafu wa jeshi la.zimamoto na uokoaji Thobias andengenye