Joy FM

M-mama yaja na suluhisho la vifo vya wajawazito, watoto

10 February 2025, 11:45

Mratibu wa huduma ya usafiri wa dharula kwa mama na mtoto M-mama  Halmashauri ya mji Kasulu Augustine Karol, Picha na Emmanuel Kamangu

Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya wameendelea kuweka mikakati ya kupata suluhisho la tatizo la vifo vya wajawazito na watoto wachanga kwa kuhakikisha huduma za dharula zinapatikana kwenye jamii.

Na Emmanuel Kamangu

Katika kukabiliana na vifo vya mama na mtoto,  mfumo jumuishi wa wa usafiri wa dharula wa  M-mama unaosaidia mama mjamzito, mama aliejifungua ndani ya siku 42 , pamoja na watoto wa changa walioko chini ya siku 28  umekuja na suruhisho la kuondokana na vifo visivyo vya lazima kwa makundi hayo.

Akizungumza na vyombo vya habari, Mratibu wa huduma ya usafiri wa dharua kwa mama na mtoto M-mama  Halmashauri ya mji kasulu Augustine Karol amesema jumla ya gari nne za kubeba wagonjwa zimetolewa  kwa kanda nne za  mji kasulu kwa ajili ya kuhudumia wajawazito,mama aliejifungua pamoja na watoto wachanga wenye vidokezo vya hatari.

Sauti ya Mratibu wa huduma ya usafiri wa dharula kwa mama na mtoto M-mama  Wialaya Kasulu Augustine Karol

Aidha Karoli amesema katika kuhakikisha mama  mjamzito na watoto wanapata huduma bora za kiafya wamekuja na utararibu wa kuwa na  dreva jamii  kwa maeneo yote ya  mji wa kasulu ili  kusaidia kusafisha wagonjwa wanaokumbana na vidokezo  hatari vinavyoweza kugarimu maisha yao.

Sauti ya Mratibu wa huduma ya usafiri wa dharula kwa mama na mtoto M-mama  Wialaya Kasulu Augustine Karol

Videkozo hatari kwa mama mjamzito na mbavyo  vinapaswa kushugulikiwa kwa wakati  ni pamoja na kupata uchungu mapema, kuvimba uso au miguu, maaumivu makali ya kichwa, maumivu makali ya tumbo huku mama mjazito dalili hatari ikiwa ni pamoja na  kutokwa damu nyingi ukeni, homa, kuoma giza na  watoto wachanga ikiwa ni kushindwa kunyonya, dege dege, kuvimba utosi pamoja na kupatwa joto kali.