Joy FM

Baraza la madiwani lapitisha bajeti ya bilioni 35 Kasulu

30 January 2025, 15:17

Madiwani katika halmashauri ya wilaya wakiwa katika kikao cha madiwani, Picha na Hagai Ruyagila

Serikalikatika halmashauri ya wilaya Kasulu imesema itaendelea kusimamia miradi ya maendeleo ili iweze kusaidia wananchi

Na Hagai Ruyagila

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma limepitisha bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 35 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri hiyo.

Bajeti hiyo imepitishwa katika kikao cha robo ya pili ya mwaka 2024/2025 katika baraza la madiwani

Katika Baraza hilo mwenyekiti wa halamshauri ya wilaya ya Kasulu ambaye pia ni diwani wa Kata ya kitanga Mh. Eliya Kagoma amewasisitiza madiwani kuwaeleza wananchi shughuli za maendeleo zinazofanywa na serikali katika maeneo yao.

Sauti ya mwenyekiti wa halamshauri ya wilaya ya Kasulu ambaye pia ni diwani wa Kata ya kitanga Mh. Eliya Kagoma

Aidha Bajeti hiyo imeonekana kugusa maeneo yote muhimu ambayo yanailenga jamii na jambo la msingi ni namna itakavyotekelezwa ili kumsaidia mwananchi wa kawaida. lakini nini maoni ya viongozi wa vyama vya siasa kuhusu Bajeti hiyo??

Sauti ya viongozi wa vyama vya siasa

Diwani wa kata ya Kigembe Simon Mpaka amesema kinachosubiriwa ni kuona ikiwa bajeti hiyo itapitishwa bungeni ili kusaidia shughuli za maendeleo kwenye kila kata.

Sauti ya Diwani wa kata ya Kigembe Simon Mpaka